Ads Here

Thursday, September 26, 2019

HUJUMA 02

Shalabah alitolewa nje ya jengo lile kwa kupitia njia ileile lakini mara hii ali[pofika kwenye ule uwa akasimama na kushangaa anachokiona, mara ya kwanza alikuta watoto wakifanya mafunzo ya kungfu na karate, lakini mara hii alikuta uwa wote umeota nyasi na wanyama kama mbuzi walikuwa wakiburudika, alishindwa kuuliza akaamua kupitiliza mpaka nje ambako aliagana na Yule msichana akalielekea gari lake. Alipoketi nyuma ya usukani ndipo alipoiona kadi ndogo nyeupe ikining’inia katika swichi ya kuwashia vifuta maji (wipers) vya gari hiyo, akainyakuwa na kuisoma.
‘…Dar es salaam Club, saa 3:00 usiku…’
Akainyakuwa na kuitia mfuko wa shati, kisha akawasha gari na kuondoka zake.
CHAPISHO LA 03
2
Makao makuu ya jwtz
Lugalo – dar es salaam
TAARIFA za kupotea kwa manowari ya jeshi la Tanzania na wapiganaji wake zilifika katika makao makuu ya jeshi hilo pale Lugalo mnamo majira ya saa tatu ausbuhi muda ambao manowari ile ilitakiwa kuwa imefika katika moja ya vituo vyake kabla ya kuwasili katika bahari ya Caspian siku mbili zinazofuata. Jeshi la Urusi lilipowasiliana na lile la Tanzania ilionekana wzi kuwa manowari hiyo imepotelea katika bahari ya Indi usiku uliotangulia, kwani kila walipojaribu kuitafuta kwa vifaa vya kisasa walishinda kabisa kuiona ilipo lakini waliweza kuona ilipoishia safari yake.
Wakipiga picha ya eneo hilo wanakuta ilikuwa sehemu za Somalia ijapokuwa ilikuwa katika maji makubwa, maji ya kimataifa.
Mkuu wa majeshi, brigedia jenerali Kamsumi alikuwa ameketi na viongozi wake wa ngazi ya juu kabisa jeshini wakijaribu kujadili juu ya upotevu wa manowari hiyo. Ulikuwa ni mkutano mzito ambao kila mshiriki alionekana kushikwa na jazba au hasira.
“Hao ni maharamia tu, si wengine, siku hizi wamekuwa wakiteka meli nyingi bila kujali sheria za kimataifa kuwa meli hizo ziko katika maji ya kimataifa, kwa nini tunawadekeza?” alilalama mmoja wa washiriki aliyekuwa katika jopo hilo.
“Meli sio tatizo, lakini vipi kuhusu makombora hayo ambayo gharama tu ya kuyatengeneza ilikuwa ni kubwa ijapokuwa tumepata ufadhili wa asilimia Fulani ya Warusi, tukiyaacha hawa jamaa si watatugeuka wenyewe?” Mjumbe mwingine alieleza.
“Hivyo vyote havina maana, wapiganaji wetu, watoto wetu wametekwa au kupotea pamoja na manowari hiyo kwa nini tuvumilie? Tuna makomandoo hapa tutume japo wawili tu wakaitafute hiyo meli kisha tuikomboe,” mjumbe wa tatu alikuwa akiongea mpaka anatoa machozi.
Baada ya majadiliano marefu na yaliyokuwa hayana mwisho, muada ulifika wa kufanya video conference na amiri jeshi mkuu. Luninga iliyokuwa ukutani ikachukua uhai na moja kwa moja mbele yao akainekana mheshimiwa Rais. Mkuu wa majeshi akaeleza kwa kifupi waliyojadiliana wajumbe katika kikao kile.
“Sikilizeni, hatuwezi kuvumilia wala kuwapa nafasi, ile ni pesa ya kodi za Watanzania, kwa nini ipotee hivihivi? Isitoshe kuna watoto wetu, vijana wetu na wapiganaji wetu, lazima waokolewe kwa gharama yeyote,” amiri jeshi mkuu aliongea kwa ukali sana, “Ninyi mna kitengo cha upelelezi ndani ya JW, haya mara moja chagueni mtu au watu wakafanye kazi hiyo, nitahitaji ripoti haraka,” mwisho wa maneno hayo ile luninga ikazimika. Kila mshiriki alishusha pumzi ndefu. Ilikuwa ni sentensi ndefu kidogo iliyowatetemesha wakuu hao wa jeshi waliokuwa wakibishana bila kupata muafaka katika lipi la kufanya. Kutokana na kauli ya aamiri jeshi mkuu, hakukuwa na mjadala mwingine kilichoangaliwa kilikuwa ni nani apewe kazi hiyo.
“Lakini jamani ee, tuiangalie hii kazi kwa ugumu na upana wake,” kiongozi mmoja alisema.
“Yeah ni kweli kuliko kudharau na kupeleka mtu ambaye atafika na kushindwa kufanya lolote. Nani tumtume akafanye kazi hiyo, kazi yan hatari kuliko hatari mwenyewe. Chekecha chekecha ikapita, Jamil Semindu, komandoo aliyemeliza mafunzo yake siku si nyingi nchini Cuba, jina lake lilipitishwa tayari kwa kazi hiyo. Mchana wa siku hiyo kijana huyo aliitwa makao makuu ya jeshi kutoka kambi ya Lugalo kule Mwenge. Naye hakukataa wito bali aliamini msemo wa wahenga, ;usikatae wito kataa neno’.
Majira ya saa nane mchana, Jamil Semindu alikuwa amesimama wima kiukakamavu mbele ya mkuu wa majeshi. Hakuwa peke yake, pembeni yake kulikuwa na mtu mwingine wa makamo, aliyavalia nguo nadhifu ya kijeshi.
“Jamil Semindu, Gwamaka Mwakajinga, tunatambua umuhimu na mchango wa kazi yenu katika jeshi letu tukufu la wananchi wa Tanzania. Nimekuiteni hapa kuwapa kazi maalum ambayo inatakiwa kuanzwa mara moja, kama mnavyojua au milivyosikia, manowari yetu ya jeshi la Tanzania, Kirov Class, ndani yake ikiwa na wapiganaji ishirini na tano pamoja na makombora kumi na mbili ya R-36 imepotea katika maji ya kimataifa huko Somalia, inahisiwa kuwa huenda ikawa imetekwa na maharamia kama iloivyotokea kwa meli zingine za mizigo. Tunawatuma muende mkafanye kazi, kwanza mkawaokoe wapiganaji wetu, pili mkaokoe makaombora yetu, tatu mkailete na meli yenyewe, mambo yote yamekwisha andaliwa mkitoka hapa tu mtaelezwa cha kufanya,” alimaliza mkuu jeshi. Wale wanajeshi wawili wakapiga salute na kisha kutoka nje ya ofisi hiyo.
Gwamaka Mwakajinga alikuwa mpelelezi wa kijeshi aliyeaminika sana hasa kwa kuzisoma nyanyo za adui, na kujua wapi alipo. Kijana huyu ndiye aliyewaongoza wenzake katika vita ya ukombozi huko visiwa vya Komoro, vita ya kumng’oa madarakani aliyekuwa rais wan chi hiyo. Alishiriki pia kupeleleza vizuri sana makazi ya waasi wa M23 pamoja na kujua maisha yao ya kila siku, mwisho wa siku aliwapa ramani yote majeshi ya Umoja wa Mataifa yakiongozwa na Tanzania na kuwafutilia mbali waasi hao. Jopo lililokaa kuchagua wawili hao liliangalia mambo mengi na tofautitofauti.
Gwamaka na Jamil wakapeana mikono na kusalimiana wakati wakiwa nje ya jengo hilo, kisha wote wawili wakaelekea katika jengo linguine kama walivyoongozwa.
“Unaonaje Meja, hawa vijana watawaweza wale maharamia wanaokunywa damu?” Luteni kanali Gogo alimuuliza mwenzake aliyekuwa naye, kapteni Kamazima.
“Wataweza tu, tuweke imani,” Meja Kamazima alimjibu.
“Maana wale maharamia kuwapata ni kazi, nao pia wamejikamilisha kwa silaha na upiganaji wa silaha,” Luteni Kanali Gogo alionesha waziwazi wasiwasi wake katika hili.
“Wataweza tu usihofu,” Meje Kamazima alimjibu na kumtia moyo mwenzake.
Taratibu zote zilikamilishwa za safari za hao jamaa, na siku iliyofuata kwa kutumia ndege ya shirika la ndege la Ethiopia waliondoka Tanzania kuelekea Somalia kupitia Addis Ababa.
“Sijacheza michezo hii siku nyingia sana,” Jamil alimwambia Gwamaka.
“Michezo midogo sana hii, nilikuwa Kivu juzijuzi tu kuwasaka M23 hivyo bado damu ya moto,” akazungumza Gwamaka. Walibadilishana mawazo wakiwa katika ndege hiyo safarini kuelekea Mogadishu.
“Sasa sikia Jamil, unajua hawa jamaa ni wajanja sana, kwa vyovyote lazima wanajua kama tunakwenda, tukifika naomba tushuke kila mtu kivyake na tusijuane isipokuwa tuwasiliane kwa simu tu kila mtu atakapofikia,” Gwamaka alijaribu kupanga mpango.
“No, tufikie hotel moja lakini tutofautishe vyumba kwa umbali mrefu kama kuna ghorofa basi mmoja ya juu mwingine ya chini,” Jamil naye akatoa pemdekezo ambalo lilikubaliwa na wote.
“Tutafanyaje operesheni yetu?” Jamil akauliza.
“Kutokana na kazi zetu, mi nitakuwa nafanya uchunguzi nakupa information na wewe unakwenda kumaliza kazi maana we ni jeshi la mtu mmoja,” wote wakacheka na kugonga viganja vyao.
RAMADA PLAZA HOTEL
Ramada plaza hoteli, ni hotel tulivu iliyo jirani na bahari katika jiji la Mogadishu, ikitazamana na bandari ya zamani ya jiji hilo. Mandhari safi, chakula na mazingira ya kuvutia viliwafanya wapiganaji hawa kuvutiwa na mahali hapo.
Alikuwa Gwamaka wa kwanza kuingia katika hotel hiyo, akapanga chumba ghorofa ya tatu juu. Baadae jamil nae akafika na kuchukua ghorofa ya chini kabisa, wakiwa tayari kikazi na wamekamilika.
Kutoka ghorofa ya tatu Gwamaka aliweza kutumia darubini yake kuangalia upande wa baharini kila baada ya nusu saa na kuandika kwenye kidaftari chake mambo anayoyajua mwenyewe. Jioni ya siku hiyo wakiwa chakulani walibadilishana mawazo hili na lile na kupanga nini cha kufanya.

No comments:

Post a Comment

Chombezo : Penzi La Shemeji Sehemu Ya Pili (2)

Nilishtuka na kutaka kukimbia ila shemeji akanishika mkono "Unakimbia nini?" aliuliza " Hapana sikimbii" nikamjibu ...