ILIKUWA HALI YA SINTOFAHAMU katika machimbo ya dhahabu huko Mashariki mwa Johanesburg, Afrika ya kusini. Katika moja ya mashimo makubwa ya tajiri maarufu, Khumalo, wafanyakazi takribani kumi na tano waliokuwa wakifanya kazi kwa ukaribu sana na mtu huyo aliyeuawa miaka kadhaa nyuma nao waliuawa na maiti zao kukutwa ndani ya mashimo hayo.
Machimbo ya dhahabu ya The Great Khumalo yalifungwa kwa muda ili kupisha uchunguzi wa mauaji hayo yaliyotokea ndani ya siku moja lakini haikujulikana ni nani hasa aliyeyatekeleza hayo. Maneno mengi sana yalisemwa na watu wa ndani na nje ya mgodi huo, lakini bado haikujulikana haswa chanzo cha vifo hivyo.
Machimbo ya dhahabu ya The Great Khumalo yalifungwa kwa muda ili kupisha uchunguzi wa mauaji hayo yaliyotokea ndani ya siku moja lakini haikujulikana ni nani hasa aliyeyatekeleza hayo. Maneno mengi sana yalisemwa na watu wa ndani na nje ya mgodi huo, lakini bado haikujulikana haswa chanzo cha vifo hivyo.
CHAPISHO LA 02
“Hatufanyi kazi mpaka tupate majibu ya vifo vya wenzetu,” mmoja wachimbaji aliyekuwa akiongoza mgomo licha ya kufungwa kwa machimbo hayo aliwaambia waandishi wa habari waliokuja kujua kulikoni.
§§§§§
Haikuwa kawaida kwa mrithi wa mgodi huo kufika katika mashimo hayo na kufanya lolote, daima alikuwa akituma watu wake wa karibu kwa kuwaunganisha na wale wa mbia wake, mzungu kutoka Canada. Lakini siku hii yeye mwenyewe aliamua kufika katika eneo hilo la machimbo.
Saa saba na nusu mchana alitua na helkopta katika viwanja hivyo na kulakiwa na mamia ya wafanyakazi wake waliokuwa wakimsubiri kwa hamu, kwa maana kuna wengine kati yao hata walikuwa hawamjui zaidi ya kusikia jina tu.
Vumbi kali lilikuwa likitimka na kufanya watu wasogee mbali na eneo hilo. Lereti Khumalo, motto wa Milionea marehemu, Khumalo au The great kama alivyopenda kujiita, alikanyaga ardhi ya uwanja huo huku akisindikizwa na wanaume watano waliokuwa kamili kila idara. Aliwekwa kati, mbele kabisa akitangulia mmoja aliyekuwa amebeba bunduki aina ya SR 2 Versek kifuani mwake, mikono yake ikiwa tayari kwa lolote. Nyuma yake walifuata vijana wawili waliovalia suti maridadi kabisa na miwani myeusi kabla ya mwenyewe Lereti ambaye nyuma yake kulikuwa na wengine wawili.
Vumbi kali lilikuwa likitimka na kufanya watu wasogee mbali na eneo hilo. Lereti Khumalo, motto wa Milionea marehemu, Khumalo au The great kama alivyopenda kujiita, alikanyaga ardhi ya uwanja huo huku akisindikizwa na wanaume watano waliokuwa kamili kila idara. Aliwekwa kati, mbele kabisa akitangulia mmoja aliyekuwa amebeba bunduki aina ya SR 2 Versek kifuani mwake, mikono yake ikiwa tayari kwa lolote. Nyuma yake walifuata vijana wawili waliovalia suti maridadi kabisa na miwani myeusi kabla ya mwenyewe Lereti ambaye nyuma yake kulikuwa na wengine wawili.
Kwa hatua za haraka kidogo huku akiwahi kulikwepa lile vumbi, Lereti alipelekwa kwenye ofisi ambayo baba yake alikuwa akiitumia sana kila aendapo kutembelea machimbo hayo. Kelele za watu waliopo nje, wakiwa na mabango, vilimsumbua mwanadada huyo mwenye miaka ishirini na nane tu. Akiwa ndani ta sueuali ya jeans iliyombana sawia, fulana nyeusi ya mikono mirefu na ilimbana shingo au tuiite kaba shingo, kofia pana aina ya pama ilikuwa kichwani kwake, kifuani alining’iniza mkufu wa uzito mkubwa wa madini ya dhahabu.
Aliketi kitini baada ya kuingia ndani ya ofisi ile na mbele yake kulikuwa na watu wawili waliokuwa na vyeo vya juu katika mgodi huo, mmoja Mwafrika akiwakilisha kampuni ya The Great Khumalo Goldmines na mwinginw Mzungu raia wa Canada anayemwakilisha mbia wake.
“Watu wanalalamika, ninyi mnajua si kawaida ya mimi kuja huku wala mshirika wangu Robinson Quebec, lakini imenilazimu kwa kuwa machozi ya wapigania uhuru yameugusa moyo wangu, name sikuwa na budi kukiuka makubaliano, niambieni tatizo liko wapi?” Lereti alianzisha mazungumzo.
“Watu wanalalamika, ninyi mnajua si kawaida ya mimi kuja huku wala mshirika wangu Robinson Quebec, lakini imenilazimu kwa kuwa machozi ya wapigania uhuru yameugusa moyo wangu, name sikuwa na budi kukiuka makubaliano, niambieni tatizo liko wapi?” Lereti alianzisha mazungumzo.
“Madam! Kama ulivyosikia, siku tatu zilizopita kuna watu kumi na tano wamepoteza maisha mgodini, na hii ndiyo wachimbaji wote wamegoma na wanataka majibu ya maswali yao,” Yule Mwafrika akajibu.
“Ok, sasa maswali hayo ni maswali gani?”
“Sisi hatuyajui, na kwa kuwa tayari kuna wakaguzi wa serikali wamekuja na kuufunga huu mgodi hivyo tunasubiri wo watasema nini,” Yule Bwana akajibu tena.
Lereti akatulia akiitazama meza, akafikiri jambo, kisha akainua uso wake na kuwatazama watu hao walio mbele yake.
“Ok, sasa maswali hayo ni maswali gani?”
“Sisi hatuyajui, na kwa kuwa tayari kuna wakaguzi wa serikali wamekuja na kuufunga huu mgodi hivyo tunasubiri wo watasema nini,” Yule Bwana akajibu tena.
Lereti akatulia akiitazama meza, akafikiri jambo, kisha akainua uso wake na kuwatazama watu hao walio mbele yake.
“Niitieni viongozi wa Wafanyakazi niongee nao, mimi ni mmoja wa wawamiliki wa mgodi huu,” Kawaeleza.
“No!” Yule Mzungu akang’aka, “Siyo utaratibu, wewe unaongea na sisi na sisi tutaongea nao,” akaongeza.
“Mmesema, wanataka majibu ya maswali yao, nimewauliza maswali ni yepi mmekiri hamuyajui, sasa mi niaongea nini na ninyi?” Lereti aliongea mpaka akapiga meza kwa ngumi, kisha akanyanyuka na kutoka nje.
Kelele za watu zilikuwa zimezidi, askari wenye mbwa walitanda kila mahali kuhakikisha hakuna vurugu yoyote itakayotokea eneo hilo. Lereti akasogea karibu na wale watu lakini akazuiliwa na askari wa Kizungu waliokuwa hapo, wakadai kwamba haruhusiwi kufanya anachokifanya.
“No!” Yule Mzungu akang’aka, “Siyo utaratibu, wewe unaongea na sisi na sisi tutaongea nao,” akaongeza.
“Mmesema, wanataka majibu ya maswali yao, nimewauliza maswali ni yepi mmekiri hamuyajui, sasa mi niaongea nini na ninyi?” Lereti aliongea mpaka akapiga meza kwa ngumi, kisha akanyanyuka na kutoka nje.
Kelele za watu zilikuwa zimezidi, askari wenye mbwa walitanda kila mahali kuhakikisha hakuna vurugu yoyote itakayotokea eneo hilo. Lereti akasogea karibu na wale watu lakini akazuiliwa na askari wa Kizungu waliokuwa hapo, wakadai kwamba haruhusiwi kufanya anachokifanya.
“Madam, hawa watu wana hasira na vifo vya ndugu zao, usiwakaribie wanaweza kukudhuru isitoshe wanajua wewe ndio mmiliki wa mgodi huu, japo si kweli,” mmoja wa askri aliyekuwa na jibwa kubwa kabisa alimwambia Lereti. Binti huyo alimtazama Mzungu Yule aliyekuwa na macho kama ya nyau.
“Pumbavu mkubwa wewe! Unaweza kunambia maneno hayo mimi, eti huu mgodi wa nani, hebu rudia…”
“Wa Sir. Robinson Quebec,” akamjibu kwa jeuri.
Lereti alimtazama na kumsonya, kisha akampita kama hamuoni.
“Madam!” akamwita huku akijaribu kumshika. Lereti akaepa na kupita lakini muda huo na nukta hiyohiyo Yule Yule bwana alichotwa ngwara maridadi kabisa na walinzi wa Lereti na kubwagwa chini.
“Pumbavu mkubwa wewe! Unaweza kunambia maneno hayo mimi, eti huu mgodi wa nani, hebu rudia…”
“Wa Sir. Robinson Quebec,” akamjibu kwa jeuri.
Lereti alimtazama na kumsonya, kisha akampita kama hamuoni.
“Madam!” akamwita huku akijaribu kumshika. Lereti akaepa na kupita lakini muda huo na nukta hiyohiyo Yule Yule bwana alichotwa ngwara maridadi kabisa na walinzi wa Lereti na kubwagwa chini.
Lereti akageuka na kurudi hatua moja mpaka kwa Yule bwana pale chini.
“Sikiliza we bwege, nakupa onyo la maneno manne tu ya kilugha chenu ‘Don’t do it again’”.
Akawaendea watu waliosimama hapo, akawatuliza na ukimya ukatawala kana kwamba hakuna mtu eneo hilo. Kisha akaomba megaphone iliyokuwa ikitumika kuwatulizia watu hao. Walipotulia kimya kabisa akaanza kuongea.
“Ndugu zangu, nimekuja hapa kuwasikiliza kilio chenu, sasa nitaruhusu maswali manne tu, na nitayajibu kwa ufasaha na nitashughuikia matatizo yenu,” akamaliza na kuwapa kipaza sauti wafanyakazi.
“Swali la msingi hapa ni moja tu, tunataka tujue sababu ya vifo mfululizo vinavyotokea hapa mgodini, mwezi uliopita vijana watano waliokuwa maopareta wa mitambo kule chini walikufa tu na hatukupewa jibu zuri, siku chache baadae kiongozi mkubwa tu katoka ofisi ya nkurugenzi amekufa ghafla ofisini kwake, na msaidizi wake siku chache baadae kapata ajali naye kafa, juzi watu kumi na tano…” alishindwa kumaliza akaanza kuliza na kile kipaaza sauti kikadakwa na mwingine.
“Sikiliza we bwege, nakupa onyo la maneno manne tu ya kilugha chenu ‘Don’t do it again’”.
Akawaendea watu waliosimama hapo, akawatuliza na ukimya ukatawala kana kwamba hakuna mtu eneo hilo. Kisha akaomba megaphone iliyokuwa ikitumika kuwatulizia watu hao. Walipotulia kimya kabisa akaanza kuongea.
“Ndugu zangu, nimekuja hapa kuwasikiliza kilio chenu, sasa nitaruhusu maswali manne tu, na nitayajibu kwa ufasaha na nitashughuikia matatizo yenu,” akamaliza na kuwapa kipaza sauti wafanyakazi.
“Swali la msingi hapa ni moja tu, tunataka tujue sababu ya vifo mfululizo vinavyotokea hapa mgodini, mwezi uliopita vijana watano waliokuwa maopareta wa mitambo kule chini walikufa tu na hatukupewa jibu zuri, siku chache baadae kiongozi mkubwa tu katoka ofisi ya nkurugenzi amekufa ghafla ofisini kwake, na msaidizi wake siku chache baadae kapata ajali naye kafa, juzi watu kumi na tano…” alishindwa kumaliza akaanza kuliza na kile kipaaza sauti kikadakwa na mwingine.
“Tuna wasiwasi hata sisi tutakufa, maana kila kif kinawagusa Waafrika tu kwani Wazungu hao hawana roho mbona hawafi, tuna wasiwasi labda kuna hujuma inayofanyika hapa mgodini, tuambiwe,” kijana huyo alipokwishakusema hayo watu wote walilipuka kwa furaha na kumshangilia.
“Mimi nataka nikuulize kimoja tu, hivi ushawahi kujiuliza kuwa kwa nini wote wnaokufa hasa wale waliokuwa ngazi za juu za uongozi ni Washririka wa mareahemu baba yako?”
Hapo moyo wa Lereti ukapiga kwa nguvu, masikio na akili yake vikafunguka, akakunja sura ya gadhabu au mshangao, hakuwahi kujiuliza kitu kama hicho wala kukifikiri, akatikisa kichwa. Kisha akaomba kipaza sauti.
“Mimi nataka nikuulize kimoja tu, hivi ushawahi kujiuliza kuwa kwa nini wote wnaokufa hasa wale waliokuwa ngazi za juu za uongozi ni Washririka wa mareahemu baba yako?”
Hapo moyo wa Lereti ukapiga kwa nguvu, masikio na akili yake vikafunguka, akakunja sura ya gadhabu au mshangao, hakuwahi kujiuliza kitu kama hicho wala kukifikiri, akatikisa kichwa. Kisha akaomba kipaza sauti.
“Nimewasikia, nimewasikia, kwa kuwa maswali yenu yote ni sawa na swali moja, naomba kwanza niwape pole waliofiwa najua wapo hapa, na kampuni itatoa rambirambi na kugharamia maazishi ya watu hao, lakini kuhusu vyanzo vya vifo hivyo ninawaahidi nitatafuta wataalamu binafsi watakaofanya uchunguzi na kisha nitawapa majibu bila kuwaicha, sintounda kamati bali nitasimamaia mwenyewe kila hatua ya uchunguzi huo. Mara baada ya serikali kumaliza uchunguzi wao ninawaomba mrudi kazini na majibu mnayoyatka mtayapata…”
Lereti alimaliza kuongea, na watu hao na kugeuka kuondoka zake akiacha nyuma yake shangwe na hoi hoi zikirindima, moja kwa moja akaelekea kwenye helkopta aliyokuja nayo na kuondoka.
Lereti alimaliza kuongea, na watu hao na kugeuka kuondoka zake akiacha nyuma yake shangwe na hoi hoi zikirindima, moja kwa moja akaelekea kwenye helkopta aliyokuja nayo na kuondoka.
§§§§§
Katikati ya watu waliokuwa kwenye kusanyiko hilo la kumsubiri na kumsikiliza Lereti alikuwapo Kachero hatari wa kike kutoka idara ya Kijasusi ya Afrika Kusini, mwanadada Debrah Mbongheni. Alisikiliza kila kilichoongelewa na akiwa katikati ya umati wa watu aliweza kudodosa hili na lile. Debrah aliitazama helkopta ile ikipotelea kwenye upeo wa macho yake, akajitoa katika lile kundi la watu na kuifuata gari yake tayari kwa swala linguine kwani ilo lilikuwa limepita.
Jioni ya siku hiyo, akiwa hotelini kwake katika vitongoji vya watu weusi huko Johanesburg, aliketi kwa utulivu juu ya kitanda kidogo akiperuzi hili na lile kuhusiana na The Great Khumalo Goldmines LTD, alkuwa akifanya chimbuchimbu kujua historia ya mgodi huo, hali ya umiliki na uendeshwaji wake kwa kupitia mtandao wa siri wa idara za usalama duniani.
Jioni ya siku hiyo, akiwa hotelini kwake katika vitongoji vya watu weusi huko Johanesburg, aliketi kwa utulivu juu ya kitanda kidogo akiperuzi hili na lile kuhusiana na The Great Khumalo Goldmines LTD, alkuwa akifanya chimbuchimbu kujua historia ya mgodi huo, hali ya umiliki na uendeshwaji wake kwa kupitia mtandao wa siri wa idara za usalama duniani.
Katika peruziperuzi hizo akjikuta akifika miaka kama mine au mitano nyuma, akasoma jinsi mauaji ya utata yaliyompata bwana Khumalo, hapo Debrah, akili na ufahamu wake vikanasa na kusoma kwa makini kabrasha hilo lililokuwa likimsisimua mwili. Hapa alimsoma mshukiwa wa mauaji Tracey Tasha. Debra akaona hapana, haitoshi, akafungua mtandao wa watu hatari duniani waliowahi kuwapo, baada ya kupita majina kadhaa kama ya kina Carlos The Jackal na wengineo, hapa akakutana na picha ya mwanamke huyo, mwembaba, mrefu, aliyeshupaa mwili, Tracy, akasoma historia yake kwa umakini sana na kugundua kuwa alikuwa ni motto wa kuasiliwa. Ijapokuwa taarifa hiyo haikueleza kwa undani sana ni nani aliyemuasili lakini iliyeleza kuwa Tracy hakusoma shule yoyote duniani, waalimu walikuwa wakija kumfundisha nyumbani na somo alilojifunza zaidi lilikuwa ni lugha, aliweza kuongea kwa ufasaha luga kumi na nne za ulimwengu.
Debra hakuamini anachokisoma alipoona kuwa kifo ca Tracy kilimfika huko Afrika ya Mashariki, Tanzania.
Debra hakuamini anachokisoma alipoona kuwa kifo ca Tracy kilimfika huko Afrika ya Mashariki, Tanzania.
“Tanzania?” akajiuliza, akuamini, akavutiwa sana kutaka kujua mwisho wa Tracy ulikuwaje huko Tanzania. Katika kupekuwa sana ndipo alipokuta abari iyo japokuwa haikuwa imeandikwa vizuri lakini alielewa kuwa Tracy aliuawa na Mpelelezi mashuhuri wa Tanzania, Afrika na nje ya mipaka ya Afrika. Hapo Debrah alijikuta akitetemeka na kichwani mwake jina la Amata au Kamanda kama aitwavyo kutokana na kazi yake inayojulikana na watu wachache lilikuwa lijirudiarudia lakini hakuweza kuona hata moja ya picha yake.
“Amata, T.S.A 1” alijiwazia jina hilo na kisha kujitupa kitandani akifikiria zaidi juu yake.
“Amata, T.S.A 1” alijiwazia jina hilo na kisha kujitupa kitandani akifikiria zaidi juu yake.
DAR ES SALAAM – saa 3:12 usiku
KAMANDA AMATA alisimama kiukakamavu mbele ya Madam S wakitenganishwa na meza kubwa iliyo katikati yao, mara hii sio ofisi kuu kule Shamba, la, ni ofisi ndogo iliyopo mita chache tu kutoka jengo muhimu kabisa la nchi hii, jengo jeupe.
Mikononi mwake alikuwa amekamata kabrasha lile ambalo Madam S jioni hiyo alikabidhiwa na Waziri wa Mambo ya Nje.
Mikononi mwake alikuwa amekamata kabrasha lile ambalo Madam S jioni hiyo alikabidhiwa na Waziri wa Mambo ya Nje.
“…anatakiwa kuuawa na si vinginevyo. Lakini kabla ya hilo Kamanda, Baraza la Usalama ya Nchi za SADC, kwa imani waliyonayo juu ya utendaji kazi wa mashirika yetu ya ndani ya usalama na kiintelijensia wametukabidhi kazi ya uchunguzi wa pili wa vifo vinavyoendelea kutukia katika moja ya migodi kule Afrika Kusini kama ilivyoandikwa humo. Ndani ya kabrasha hilo utapata taarifa ya uchunguzi uliofanywa na shirika Fulani la Afrika ya Kusini lakini SADC haijaridhika nao, hivyo imeomba kazi hii ifanywe na idara za hapa nchini, yaani nje ya Afrika Kusini, kazi hii ni siri na ombi hili ni siri kubwa.
Kwa kifupi, uwende Afrika ya Kusini, ukakamilishe zoezi hilo kwa siku chache, kisha kama huyo anayetajwa humo ndiye, basi unatakiwa kuhakikisha ameuawa kwa siri ikishindikana utajua wewe, Afrika imechoka.”
Kamanda Amata akiwa kalibana kabrasha lile kwa mkono wake mmoja wa kushoto, alimtazama Madam S kwa macho makavu.
Kamanda Amata akiwa kalibana kabrasha lile kwa mkono wake mmoja wa kushoto, alimtazama Madam S kwa macho makavu.
“Kamanda Amata, nategemea utafanya kazi hiyo kwa uaminifu mkubwa kuliko siku zote, unapoona Jumuiya kubwa kama hizi zinakutumia ujue wewe sasa ni zaidi ya T.S.A 1. Uwe makini kwani ukichelea, Makaburu hawana mzaha, maisha yako rehani sasa, nakusubiri kwenye meza hii hii ama ukiwa hivyo ulivyo au ukiwa ndani ya box,” Madam S akamaliza.
Kamanda Amata akasimama kwa ukakamavu, “Yes, Madam, umesomeka, kazi itafanyika”. Wakapeana mikono, Madam S akazunguka upande wa pili na kumkumbatia Kamanda huku machozi yakimtoka.
“Nakupenda Amata, nakupenda zaidi ya mtoto au mume wangu,”…
Kamanda Amata akasimama kwa ukakamavu, “Yes, Madam, umesomeka, kazi itafanyika”. Wakapeana mikono, Madam S akazunguka upande wa pili na kumkumbatia Kamanda huku machozi yakimtoka.
“Nakupenda Amata, nakupenda zaidi ya mtoto au mume wangu,”…
INAENDELEA…..
No comments:
Post a Comment