SEHEMU YA NNE – PART 1
Na sasa Max yuko Tanzania, Arusha, kwa kazi maalum kama mwenyewe anavyosema.
“Najua afande kisha changanyikiwa hadi sasa. Nyie endeleeni na shughuli nyingine na kupata muda wa kupumzika. Kazi tuliyofanya hadi sasa inaridhisha sana. Nitawapa taarifa wakubwa kuwa tumeshaanza kuitingisha Arusha, lakini najua hata kabla sijawapatia watakuwa wameshaanza kuzipata kupitia vyombo vya habari. Kwa sasa macho yangu na masikio yangu mawili nayaelekeza kwa Mzee Edson Kinyaro. Najua atakuwa ameshajua kuwa niko hapa mjini kutokana na alama fulani ambayo nimekuwa nikiiacha katika maeneo ya tukio. Katika wapelelezi wote tunaotakiwa kuwaua, kazi kubwa itakuwa namna ya kumuua Jacob Matata. This is my old friend, work mate na pia mwalimu wetu ni mmoja. Ila najua namzidi uzoefu, yeye ameendelea kuwa malaika wakati miye ni shetani sasa. Najua Edson anajua kama kuna mtu wa kuweza kunidhibiti miye kwa lolote nililokusudia kufanya, japo hajui ni nini nataka kufanya, basi mtu huyo ni Jacob Matata. Hatutakiwi kuwauwa Inspekta Sogoyo na Edson Kinyaro kwa sasa. Inspekta Sogoyo tunamwacha hai ili aendelee kueneza habari zetu. Edson tunamwacha ili atusaidie kupata nyendo za Jacob Matata. Akishatuletea tu Jacob Matata basi tunammaliza Edson na Matata pamoja. Nadhani hadi hapo tutakuwa tumemaliza kazi kwa awamu ya kwanza” Max alielezea, wakati huu alikuwa ameshamaliza kusafisha bastola yake.
* * *
Siku iliyofuata yaani Ijumaa ya Julai 17, 2009 majira ya jioni, tetesi ya kwanza ilipomfikia Jacob Matata hakushtuka sana kwa sababu hakuipa uzito, kwani aliyeitoa hakumwamini vilivyo. Jambo jingine ni kwamba isingekuwa busara kwa mpelelezi wa hadhi kama yake kuamini mara moja maneno ya kijiweni. Mkusanyiko wa vijana mtaani usio rasmi kwa ajili ya kusimuliana mambo mbalimbali ya kila siku, wenyewe huuita Kijiwe. Kijiwe kilichotumiwa na vijana hawa kilikuwa maeneo ya Kinondoni-Mkwajuni pembezoni mwa baa moja maarufu sana eneo hilo iitwayo Ufipa Bar. Hapo ndipo Jacob alipohakikisha kuwa anajichanganya na vijana hao ili kupata habari mbalimbali zihusuzo vijana na jamii kwa ujumla.
Pamoja na kuwa alikuwa ni mtu mwenye majukumu mengi na muhimu, Jacob Matata bado alikuwa akiamini jambo moja, nalo ni kuwa; kama unataka kutatua matatizo yanayoikabili jamii basi huna budi uwe na muda wa kukaa na jamii hiyo. Aliamini kuwa fimbo ya mbali haiuwi nyoka. Nadhalia hii ndiyo iliyomfanya atenge muda wake kwenda kukaa kijiweni kila apatapo nafasi mida ya jioni. Japo alionekana kuwa na ufahamu wa juu kuliko wao, lakini vijana wenzie hawakusita kumshirikisha na kujadili mambo kadha wa kadha pamoja naye. Hawakukosekana waliomtilia shaka juu ya uamuzi wake wa kujichanganya pamoja nao. Sababu kuu ni kwa vile vijana wengi wenye hadhi kama yake hawakuwa na desturi ya kukaa kijiweni hapo. Wamekuwa wakijitenga na jamii ya chini kwa kigezo kuwa kukuaa nayo wala haikuongezei kitu chochote – Hwana mawazo. Huku wakisahau kuwa ustawi wao hao vijana wanaojiita wameendelea kwa kiasi kikubwa unategemea utengemavu wa hawa vijana wa kijiweni. Pia Jacob aliamini kuwa kama vijana walio elimika na kuafikiwa kimaisha wakijitenga na wale ambao hawako vema je nani atawasaidia hawa ambao bado hawajatoka, hata kimawazo tu.
“Ee bwana ee hii nchi imevamiwa”. Alianza Idrisa kijana ambaye alikuwa maarufu kwa michapo ambayo isingekuwa rahisi wenzie kuipata. Alisita kidogo wakati Jacob alipowasili kijiweni hapo na kuwasalimia wote kabla hajachukua jiwe lililokuwa pembeni na kutia kitako.
“Eee, kwani vipi mshikaji Idrisa?” Mmoja alidadisi katika hali ya kumtaka Idrisa aendelee.
“Kuna skendo moja nimeipata inashangaza”. Alitulia kidogo. “Nasikia kuna watu fulani kutoka mamtoni wameingia hapa nchini wakiwa na silaha za maangamizi, silaha hizo ni za vijidudu ambazo huwa mnasikia zinatengenezwa huko mamtoni. Sasa jamaa wamekuja nazo huku ili kuzifanyia majaribio...” Alisema Idrisa huku akiomba aongezewe kahawa katika kikombe chake.
“Hiyo haiwezekani, we unafikiri hii nchi haina ulinzi? Isitoshe silaha hizo ni hatari sana, ikipigwa kama hapa inaweza kumaliza nchi nyingi sana kwa muda mfupi” mmoja alipinga huku wengine wakitingisha vichwa kama ishara ya kuafikiana na huyu aliyepinga.
“Jamani tusimpinge Idrisa kwani hatuwezi kujua mchapo huu kautoa wapi. Kwani we Idrisa hii skendo umeipata wapi? Hatimaye Jacob aliingilia huku akiwa na hamu ya kujua huyu kijana alikuwa amepata wapi taarifa hizo za kusisimua.
Weee braza Sam, achana nao hawa, jana nilimsikia baba akiwa anaongelea mambo haya…” Katika kijiwe hiki Jacob alijitambulisha kwa jina la Sam.
“Idrisa acha, hata kama dingi yako ni kigogo serikalini lakini mara nyingine unataka kutufunga kamba kwa kisingizio cha - baba yako kasema”. Huyu aliyeonekana kuwa kinyume na Idrisa alipinga tena.
“Kwa hiyo hao jamaa wako hapa hapa mjini au kwingineko? Jacob Aliuliza
“inasemekana wameenda mji mwingine, nahisi wameona hapa jijini itakuwa rahisi kushitukiwa” Kwa jinsi Idrisa alivyokuwa akielezea ilikuwa wazi kuwa mchapo huo hakuwa ameubuni, japo wenzake wote walionekana kutokuwa na imani naye hata kidogo. Jacob kwa upande wake hakuyabeza wala kuyapa uzito mkubwa maelezo hayo.
Baada ya hayo zilifuata stori za hapa na pale ambazo Jacob hakuona kama angeendelea kuzipa muda wa kusikiliza, aliondoka zake baada ya kuwa amelipa bili yote ya kahawa kwa wote waliokuwa hapo. Vijana kijiweni walifurahi baada ya kulipiwa na Jacob, hii ilikuwa moja ya sababu za wao kumpenda sana pale kijiweni.
“Najua afande kisha changanyikiwa hadi sasa. Nyie endeleeni na shughuli nyingine na kupata muda wa kupumzika. Kazi tuliyofanya hadi sasa inaridhisha sana. Nitawapa taarifa wakubwa kuwa tumeshaanza kuitingisha Arusha, lakini najua hata kabla sijawapatia watakuwa wameshaanza kuzipata kupitia vyombo vya habari. Kwa sasa macho yangu na masikio yangu mawili nayaelekeza kwa Mzee Edson Kinyaro. Najua atakuwa ameshajua kuwa niko hapa mjini kutokana na alama fulani ambayo nimekuwa nikiiacha katika maeneo ya tukio. Katika wapelelezi wote tunaotakiwa kuwaua, kazi kubwa itakuwa namna ya kumuua Jacob Matata. This is my old friend, work mate na pia mwalimu wetu ni mmoja. Ila najua namzidi uzoefu, yeye ameendelea kuwa malaika wakati miye ni shetani sasa. Najua Edson anajua kama kuna mtu wa kuweza kunidhibiti miye kwa lolote nililokusudia kufanya, japo hajui ni nini nataka kufanya, basi mtu huyo ni Jacob Matata. Hatutakiwi kuwauwa Inspekta Sogoyo na Edson Kinyaro kwa sasa. Inspekta Sogoyo tunamwacha hai ili aendelee kueneza habari zetu. Edson tunamwacha ili atusaidie kupata nyendo za Jacob Matata. Akishatuletea tu Jacob Matata basi tunammaliza Edson na Matata pamoja. Nadhani hadi hapo tutakuwa tumemaliza kazi kwa awamu ya kwanza” Max alielezea, wakati huu alikuwa ameshamaliza kusafisha bastola yake.
* * *
Siku iliyofuata yaani Ijumaa ya Julai 17, 2009 majira ya jioni, tetesi ya kwanza ilipomfikia Jacob Matata hakushtuka sana kwa sababu hakuipa uzito, kwani aliyeitoa hakumwamini vilivyo. Jambo jingine ni kwamba isingekuwa busara kwa mpelelezi wa hadhi kama yake kuamini mara moja maneno ya kijiweni. Mkusanyiko wa vijana mtaani usio rasmi kwa ajili ya kusimuliana mambo mbalimbali ya kila siku, wenyewe huuita Kijiwe. Kijiwe kilichotumiwa na vijana hawa kilikuwa maeneo ya Kinondoni-Mkwajuni pembezoni mwa baa moja maarufu sana eneo hilo iitwayo Ufipa Bar. Hapo ndipo Jacob alipohakikisha kuwa anajichanganya na vijana hao ili kupata habari mbalimbali zihusuzo vijana na jamii kwa ujumla.
Pamoja na kuwa alikuwa ni mtu mwenye majukumu mengi na muhimu, Jacob Matata bado alikuwa akiamini jambo moja, nalo ni kuwa; kama unataka kutatua matatizo yanayoikabili jamii basi huna budi uwe na muda wa kukaa na jamii hiyo. Aliamini kuwa fimbo ya mbali haiuwi nyoka. Nadhalia hii ndiyo iliyomfanya atenge muda wake kwenda kukaa kijiweni kila apatapo nafasi mida ya jioni. Japo alionekana kuwa na ufahamu wa juu kuliko wao, lakini vijana wenzie hawakusita kumshirikisha na kujadili mambo kadha wa kadha pamoja naye. Hawakukosekana waliomtilia shaka juu ya uamuzi wake wa kujichanganya pamoja nao. Sababu kuu ni kwa vile vijana wengi wenye hadhi kama yake hawakuwa na desturi ya kukaa kijiweni hapo. Wamekuwa wakijitenga na jamii ya chini kwa kigezo kuwa kukuaa nayo wala haikuongezei kitu chochote – Hwana mawazo. Huku wakisahau kuwa ustawi wao hao vijana wanaojiita wameendelea kwa kiasi kikubwa unategemea utengemavu wa hawa vijana wa kijiweni. Pia Jacob aliamini kuwa kama vijana walio elimika na kuafikiwa kimaisha wakijitenga na wale ambao hawako vema je nani atawasaidia hawa ambao bado hawajatoka, hata kimawazo tu.
“Ee bwana ee hii nchi imevamiwa”. Alianza Idrisa kijana ambaye alikuwa maarufu kwa michapo ambayo isingekuwa rahisi wenzie kuipata. Alisita kidogo wakati Jacob alipowasili kijiweni hapo na kuwasalimia wote kabla hajachukua jiwe lililokuwa pembeni na kutia kitako.
“Eee, kwani vipi mshikaji Idrisa?” Mmoja alidadisi katika hali ya kumtaka Idrisa aendelee.
“Kuna skendo moja nimeipata inashangaza”. Alitulia kidogo. “Nasikia kuna watu fulani kutoka mamtoni wameingia hapa nchini wakiwa na silaha za maangamizi, silaha hizo ni za vijidudu ambazo huwa mnasikia zinatengenezwa huko mamtoni. Sasa jamaa wamekuja nazo huku ili kuzifanyia majaribio...” Alisema Idrisa huku akiomba aongezewe kahawa katika kikombe chake.
“Hiyo haiwezekani, we unafikiri hii nchi haina ulinzi? Isitoshe silaha hizo ni hatari sana, ikipigwa kama hapa inaweza kumaliza nchi nyingi sana kwa muda mfupi” mmoja alipinga huku wengine wakitingisha vichwa kama ishara ya kuafikiana na huyu aliyepinga.
“Jamani tusimpinge Idrisa kwani hatuwezi kujua mchapo huu kautoa wapi. Kwani we Idrisa hii skendo umeipata wapi? Hatimaye Jacob aliingilia huku akiwa na hamu ya kujua huyu kijana alikuwa amepata wapi taarifa hizo za kusisimua.
Weee braza Sam, achana nao hawa, jana nilimsikia baba akiwa anaongelea mambo haya…” Katika kijiwe hiki Jacob alijitambulisha kwa jina la Sam.
“Idrisa acha, hata kama dingi yako ni kigogo serikalini lakini mara nyingine unataka kutufunga kamba kwa kisingizio cha - baba yako kasema”. Huyu aliyeonekana kuwa kinyume na Idrisa alipinga tena.
“Kwa hiyo hao jamaa wako hapa hapa mjini au kwingineko? Jacob Aliuliza
“inasemekana wameenda mji mwingine, nahisi wameona hapa jijini itakuwa rahisi kushitukiwa” Kwa jinsi Idrisa alivyokuwa akielezea ilikuwa wazi kuwa mchapo huo hakuwa ameubuni, japo wenzake wote walionekana kutokuwa na imani naye hata kidogo. Jacob kwa upande wake hakuyabeza wala kuyapa uzito mkubwa maelezo hayo.
Baada ya hayo zilifuata stori za hapa na pale ambazo Jacob hakuona kama angeendelea kuzipa muda wa kusikiliza, aliondoka zake baada ya kuwa amelipa bili yote ya kahawa kwa wote waliokuwa hapo. Vijana kijiweni walifurahi baada ya kulipiwa na Jacob, hii ilikuwa moja ya sababu za wao kumpenda sana pale kijiweni.
* * *
Siku iliyofuata yaani Julai 18, 2009, tetesi hizo zililifikia tena sikio lake, safari hii ziliupekenya Moyo wake na kumweka katika hali tofauti. Jacob Matata alipata taarifa rasmi. Ilikuwa ni siku moja tu tangu alipopata tetesi toka kwa Idrisa pale kijiweni maeneo ya Ufipa Bar.
Siku hii akiwa ofisini kwake alipokea simu toka kwa mkurugenzi wa Ofisi Fukuzi, Bi. Anita. Simu hii ilikuwa ni ya wito wa haraka ambapo Jacob alihitajika ofisini kwa mkurugenzi huyo. Alipofika ofisini kwa Bi. Anita alimkuta akimsubiri. Bi. Anita alikuwa katika suti nyeusi ya kike iliyomfanya apendezeshe ofisi hiyo. Alipomwona Jacob akiingia alitabasamu na kujitengeneza vizuri kitini.
"Keti Jacob" Alisema huku akitoa karatasi fulani toka katika uvungu wa meza yake.
“Asante” Jacob alisema huku akivuta kiti kabla ya kuketi.
“Nimekuita hapa kufuatia dharura iliyojitokeza”. Bi. Anita alirekebisha sauti yake, kisha akaendelea
“Siku chache zilizopita kumekuwa na taarifa kuwa kuna kundi la watu ambalo limeingia Nchini kwa siri. Kundi hilo limeingia likiwa na silaha na inaaminika kuwa silaha hizo ni za nchi za magharibi. Watu hawa wametumwa na Nchi hizo kwa lengo la kuzifanyia majaribio. Haijulikani kwa nini watu hawa wameamua kuja kuzifanyia majaribio hapa nchini wakati kwa kawaida watu hawa hufanya majaribio baharini, misituni na sehemu zinazofanana na hizo. Uhakika uliopo na jambo la kusikitisha ni kuwa, silaha hizo hazitafanyiwa majaribio kwenye mojawapo ya misitu, mbuga, au maeneo wazi yaliyopo hapa nchini. Bali wanataka kufanya majaribio kwa kutumia viumbe hai – raia wa Tanzania. Kwa kuona kuwa maisha ya watu wetu hayana thamani sawa na yale ya watu wao, nchi hizo zilizoendelea zimeona kuwa majaribio haya yatakuwa ya mafanikio kama yakifanyika kwetu. Habari zisizo rasmi zinadai kuwa watu hao tayari wapo Arusha. Bila shaka wameuchagua mji huo kwa kuanza kufanya kazi yao.
Inawezekana umeshasikia jinsi walivyouawa wale madaktari sita, askari kumi na moja, na vichaa saba huko Arusha ndani ya siku chache hizi. Ni baada ya watu hao kwenda kwenye Hospital ya mkoa wa Arusha Mount Meru na kutumia silaha hizo hatari. Kama ujuavyo mji wa Arusha hivi karibuni utakuwa mwenyeji wa mkutano mmoja muhimu, lakini watu wasiojulikana wamesambaza barua za kutishia mkutano huo. Leo asubuhi nimepokea taarifa toka kwa mheshimiwa kunitaka kuhakikisha kuwa watu hao wanapatikana haraka iwezekanavyo.
Kama ujuavyo hii ndiyo ofisi inayotegemewa kwa maswala yaliyoshindikana na nyeti kama haya. Bila shaka unamjua vema Mheshimiwa kwa jinsi alivyo, asingependa kuona watu wakizidi kuteketea, huku kukiwa na tishio la silaha hatari kama ambazo inasemekana watu hao wanazo. Pia itakuwa aibu sana kama mkutano uliopangwa kufanyika hautafanyika kwa sababu ya vitisho toka kwa wahuni kama hao…..”
“Lakini kuna hakika gani kuwa jamaa walioingia na silaha ndiyo hao hao waliotishia mkutano? Jacob aliuliza katika hali ya kuunganisha mambo
“Haijawahi tokea watu kutishia mkutano wa kimataifa katika nchi hii. Hii ni mara ya kwanza na imetokea wakati watu hao wameingia nchini na wameshafanya mauaji ya kutisha. Hivyo kwa akili ya kawaida sana, wamehusishwa moja kwa moja na vitisho vilivyotolewa. Lakini ushahidi wazi kabisa ni kuwa mmoja kati ya askari waliouawa jana, pembeni ya maiti yake pia ulikutwa ujumbe wa kutishia mkutano. Kutokana na kazi waliyoifanya juzi katika hospitali ya mkoa walipokwenda, imethibitika kuwa watu hao wamekuja na silaha za kisasa. Si hivyo tu bali imethibitika pia kuwa wanauwezo wa hali ya juu katika mapigano. Binafsi kilichonishangaza ni kitendo cha watu hawa kutaka kuingilia na kuvuruga mkutano muhimu huu uliopangwa kufanyika kwenye moja ya miji yetu siku chache zijazo.
Mtazamo wangu katika suala hili ni kwamba kuna jambo limefichika juu ya watu hao wanaodaiwa kuingia nchini na ambao tayari wameshaanza kufanya ukatili wa kutisha. Ninahisi kuna jambo jingine zaidi ya lile la kutaka kufanyia majaribio silaha zao. Kwa nini waamue kufika kipindi ambacho mkutano huu umekusudiwa kufanywa na waingie moja kwa moja nchini mwetu na si kwingineko katika bara hili la Africa….” Kabla hajaendelea alikatizwa na swali la Jacob.
“Bosi kwani silaha hizo ni za aina gani mpaka waamue kuja kufanyia hapa nchini na si kwao. Na je watu hao ni waafrika au wazungu? Jacob aliuliza huku amekaza macho yake yakitazamana na yale ya Bi. Anita.
“Watu walioingia hapa nchini si wazungu ni waafrika ambao bila shaka wametumika kama vibaraka wa wazungu. Kwa vile silaha hizo ni za hatari sana, ndio maana waliozitengeneza wameogopa kuzifanyia majaribio huko kwao. Kwani taarifa tulizonazo toka Arusha kwa wataalamu wetu zinasema ni silaha za kibaiolojia ambazo huathiri kabisa mfumo mzima wa mwili wa binadamu.
Siku iliyofuata yaani Julai 18, 2009, tetesi hizo zililifikia tena sikio lake, safari hii ziliupekenya Moyo wake na kumweka katika hali tofauti. Jacob Matata alipata taarifa rasmi. Ilikuwa ni siku moja tu tangu alipopata tetesi toka kwa Idrisa pale kijiweni maeneo ya Ufipa Bar.
Siku hii akiwa ofisini kwake alipokea simu toka kwa mkurugenzi wa Ofisi Fukuzi, Bi. Anita. Simu hii ilikuwa ni ya wito wa haraka ambapo Jacob alihitajika ofisini kwa mkurugenzi huyo. Alipofika ofisini kwa Bi. Anita alimkuta akimsubiri. Bi. Anita alikuwa katika suti nyeusi ya kike iliyomfanya apendezeshe ofisi hiyo. Alipomwona Jacob akiingia alitabasamu na kujitengeneza vizuri kitini.
"Keti Jacob" Alisema huku akitoa karatasi fulani toka katika uvungu wa meza yake.
“Asante” Jacob alisema huku akivuta kiti kabla ya kuketi.
“Nimekuita hapa kufuatia dharura iliyojitokeza”. Bi. Anita alirekebisha sauti yake, kisha akaendelea
“Siku chache zilizopita kumekuwa na taarifa kuwa kuna kundi la watu ambalo limeingia Nchini kwa siri. Kundi hilo limeingia likiwa na silaha na inaaminika kuwa silaha hizo ni za nchi za magharibi. Watu hawa wametumwa na Nchi hizo kwa lengo la kuzifanyia majaribio. Haijulikani kwa nini watu hawa wameamua kuja kuzifanyia majaribio hapa nchini wakati kwa kawaida watu hawa hufanya majaribio baharini, misituni na sehemu zinazofanana na hizo. Uhakika uliopo na jambo la kusikitisha ni kuwa, silaha hizo hazitafanyiwa majaribio kwenye mojawapo ya misitu, mbuga, au maeneo wazi yaliyopo hapa nchini. Bali wanataka kufanya majaribio kwa kutumia viumbe hai – raia wa Tanzania. Kwa kuona kuwa maisha ya watu wetu hayana thamani sawa na yale ya watu wao, nchi hizo zilizoendelea zimeona kuwa majaribio haya yatakuwa ya mafanikio kama yakifanyika kwetu. Habari zisizo rasmi zinadai kuwa watu hao tayari wapo Arusha. Bila shaka wameuchagua mji huo kwa kuanza kufanya kazi yao.
Inawezekana umeshasikia jinsi walivyouawa wale madaktari sita, askari kumi na moja, na vichaa saba huko Arusha ndani ya siku chache hizi. Ni baada ya watu hao kwenda kwenye Hospital ya mkoa wa Arusha Mount Meru na kutumia silaha hizo hatari. Kama ujuavyo mji wa Arusha hivi karibuni utakuwa mwenyeji wa mkutano mmoja muhimu, lakini watu wasiojulikana wamesambaza barua za kutishia mkutano huo. Leo asubuhi nimepokea taarifa toka kwa mheshimiwa kunitaka kuhakikisha kuwa watu hao wanapatikana haraka iwezekanavyo.
Kama ujuavyo hii ndiyo ofisi inayotegemewa kwa maswala yaliyoshindikana na nyeti kama haya. Bila shaka unamjua vema Mheshimiwa kwa jinsi alivyo, asingependa kuona watu wakizidi kuteketea, huku kukiwa na tishio la silaha hatari kama ambazo inasemekana watu hao wanazo. Pia itakuwa aibu sana kama mkutano uliopangwa kufanyika hautafanyika kwa sababu ya vitisho toka kwa wahuni kama hao…..”
“Lakini kuna hakika gani kuwa jamaa walioingia na silaha ndiyo hao hao waliotishia mkutano? Jacob aliuliza katika hali ya kuunganisha mambo
“Haijawahi tokea watu kutishia mkutano wa kimataifa katika nchi hii. Hii ni mara ya kwanza na imetokea wakati watu hao wameingia nchini na wameshafanya mauaji ya kutisha. Hivyo kwa akili ya kawaida sana, wamehusishwa moja kwa moja na vitisho vilivyotolewa. Lakini ushahidi wazi kabisa ni kuwa mmoja kati ya askari waliouawa jana, pembeni ya maiti yake pia ulikutwa ujumbe wa kutishia mkutano. Kutokana na kazi waliyoifanya juzi katika hospitali ya mkoa walipokwenda, imethibitika kuwa watu hao wamekuja na silaha za kisasa. Si hivyo tu bali imethibitika pia kuwa wanauwezo wa hali ya juu katika mapigano. Binafsi kilichonishangaza ni kitendo cha watu hawa kutaka kuingilia na kuvuruga mkutano muhimu huu uliopangwa kufanyika kwenye moja ya miji yetu siku chache zijazo.
Mtazamo wangu katika suala hili ni kwamba kuna jambo limefichika juu ya watu hao wanaodaiwa kuingia nchini na ambao tayari wameshaanza kufanya ukatili wa kutisha. Ninahisi kuna jambo jingine zaidi ya lile la kutaka kufanyia majaribio silaha zao. Kwa nini waamue kufika kipindi ambacho mkutano huu umekusudiwa kufanywa na waingie moja kwa moja nchini mwetu na si kwingineko katika bara hili la Africa….” Kabla hajaendelea alikatizwa na swali la Jacob.
“Bosi kwani silaha hizo ni za aina gani mpaka waamue kuja kufanyia hapa nchini na si kwao. Na je watu hao ni waafrika au wazungu? Jacob aliuliza huku amekaza macho yake yakitazamana na yale ya Bi. Anita.
“Watu walioingia hapa nchini si wazungu ni waafrika ambao bila shaka wametumika kama vibaraka wa wazungu. Kwa vile silaha hizo ni za hatari sana, ndio maana waliozitengeneza wameogopa kuzifanyia majaribio huko kwao. Kwani taarifa tulizonazo toka Arusha kwa wataalamu wetu zinasema ni silaha za kibaiolojia ambazo huathiri kabisa mfumo mzima wa mwili wa binadamu.
ITAENDELEA……
No comments:
Post a Comment