Ndiyo, sikuwa namjua kabla ila baada ya kuuwawa na Jacob Matata, ndiyo nikajua kuwa alikuwa naitwa Ben au Kiroboto!!!! Inspekta Sogoyo alisema.
“Basi huyo pia alikuwa kijana wangu japo alipokwenda kwenye mafunzo ya mwisho hakurudi tena Tanzania na wala sikuwa na taarifa zake. Kwa hiyo kati ya hawa watatu waliotoweka na ambao hatujui kama wamekufa au la mmoja alikuwa anapenda sana kutumia alama ya Sungura aliyefumba macho kama alama yake. Bila shaka unaelewa sifa za Sungura; akiwa amefumba macho ina maana hajalala, na macho yakiwa yamefumbuliwa ina maana amelala. Sungura anajiamini kwa mbio fupifupi na haoni shida kuwa jirani na adui maana anajiamini kwa chenga. Hizo ndiyo zilikuwa sifa za huyo kijana wangu. Yeye alikuwa hamkwepi adui hata siku moja, alikuwa akiwasaka na kuwafuata hadui katika himaya zao. Kijana huyu alikuwa mjanja kupindukia, kama Sungura. Kwa hii alama na vitendo vilivyokwisha fanyika, nina hakika kabisa kuwa huyu kichaa yuko hapa mjini. Na kama yuko hapa mjini basi kazi ipo kweli kweli. Inabidi ujipange sawa sawa Sogoyo…..”
“Jina lake halisi anaitwa nani? Inspekta Sogoyo aliuliza
“Mtu akishaondoka kwenye timu na tukawa tunajua ni mtu hatari sana, jina lake linabaki kuwa kitu cha siri ambacho kitafia vifuani mwa wanaojua. Tunafanya hivi ili hata ikitokea akafanya madhambi nchi nyingine hatutaki wamuhusishe na sisi. Huwa tunaharibu jina lake katika kumbukumbu zote ambazo limewahi kuwepo. Hivyo jibu naloweza kukupa ni…sijui jina lake halisi”
“Kwa hiyo kati ya vijana wako safi watano hakuna hata mmoja aliyebaki kuwa msafi? Inspekta Sogoyo alihoji huku akishusha pumzi.
“Aliyemuua Kiroboto mwaka jana yeye ndiye pekee aliyebaki upande wa serikali japo si rahisi kumpata maana hajihusishi na serikali moja kwa moja, mmoja atakuwa ndiyo huyu ambaye unatakiwa ukabiliane naye hapa Arusha sasa, wengine wawili sijui wako wapi na sijui majina yao kama nilivyokuambia. Mmoja ndiyo aliuawa mwaka jana” Edson alisema huku akijinyoosha na kisha kumimina kahawa kwenye kikombe.
“Haina shida nadhani tunaweza kabiliana naye tu, tutamshinda tu. Nikimpata nitamfikishia salamu zako kabla sijaweka risasi ya mwisho kwenye kichwa chake. Maana mijitu kama hiyo ukiipata unaua pale pale halafu unaandaa sababu safi za kuhalalisha kitendo chako” Inspekta Sogoyo aliongea kwa sauti ya jazba kidogo.
“Naomba Mungu mumpate, na kama kweli ukimpata mfikishie salamu kama ulivyosema. Ila najua haitakuwa kazi rahisi, kumbuka hapa mnapambana na mtu mwenye uwezo wa kumaliza kikosi cha jeshi la watu Mia moja yeye peke yake. Ninaposema vijana safi namaanisha walikuwa vijana safi, ambao Nyerere mwenyewe alikuwa anaelewa kuwa ana watu kama hao….”
“Sasa mzee Edson naona unanitisha sasa” Sogoyo alifoka.
“Sikutishi, nakuambia hali halisi, kumjua mpinzani wako inasemekana ni nusu ya ushindi. Nakuambia hivi ili ujue namna ya kupambana na huyu mtu. Hata miye najuta kwa nini niliwaacha hai hawa vijana, nadhani kuwaacha hai lilikuwa ni kosa la kifundi ambalo madhara yake nayaona sasa” Mzee Edson aliongea kwa unyonge na sauti ya kusononeka.
“Tutampata tuu, wala usijali. Miye Sogoyo. Nina timu ya vijana safi ambao kwa pamoja tunaweza utifua mjiu huu juu chini hadi mtu wako apatikane. Labda akimbie mji mambo yakishamkalia vibaya, la, nitakuletea kichwa chake hapa utoe salamu za mwisho!!!!
Inspekta Sogoyo alisema huku akiwa anainuka tayari kwa kuondoka.
“Nani wa kukimbia? Edson aliuliza kwa sauti ya chini
“Huyo mtu wako” Sogoyo alisema
“Inspekta, kuwa makini kijana wangu, unaingia kupambana na fundi hasa” Edson alisema, kisha akaongeza.
“Yule ni mtu ambaye kama anakutaka hata wewe anaweza kukufuata kituoni, ukiwa umezungukwa na askari wako”
“Inaonekana wamfagilia sana huyo mtu wako!!! Sogoyo alisema kwa sauti ya mashaka kidogo.
“Sogoyo, usipoteze moyo wa mapambano, wakati mambo yanapokuwa magumu ndipo tunapoweza kuwatambua watu wagumu pia. Nakutakia mafanikio katika kazi yako, ila kuwa makini sana kwa kila ufanyalo kuanzia sasa” Mzee Edson Kinyaro alisema kisha wakapeana mikono kama ishara ya kuagana.
“Je, wahitaji kubaki na hii karatasi? Sogoyo aliuliza
“Hapana, kwenye kazi zetu tulikuwa hatupendi kukaa na ushahidi bila sababu” Mzee Edson alisema huku akiwa anaifinyanga ile karatasi yenye mchoro wa Sungura aliyefumba macho, akaitupia kwenye moto.
Ilikuwa inagota saa moja kasoro dakika sita jioni wakati ambapo Inspekta Sogoyo alipokuwa akiondoka nyumbani kwa Edson Kinyaro, mkuu wa zamani wa idara ya usalama wa Taifa.
Sogoyo alipoondoka, Edson alijibwaga kwenye moja ya sofa zilizokuwa pale sebuleni, huku akionekana mwingi wa mawazo.
“Shiiiit, Max amekuja Tanzania kutafuta nini!!!!!! Edson alijikuta akiwaza kwa sauti. “Mbona hatari sana, kuna jambo kubwa linaendelea hapa Arusha, Max hawezi kuja Arusha hivi hivi. Mshenzi huyu huwa akianza kuua huwa inakuwa nghumu sana kupata namna ya kumzuia, any way dawa yake ni moja tu……!!!!! Edson aliendelea kuwaza kwa sauti huku safari hii akiwa anajizoa zoa toka pale kwenye sofa alipokuwa amejibwaga hapo awali.
“Ama kweli, hata kama mavi ya kale hayanuki lakini bado ni najisi” Alijisemea mzee Edson huku akinyanyua kikombe cha kahawa.
“Basi huyo pia alikuwa kijana wangu japo alipokwenda kwenye mafunzo ya mwisho hakurudi tena Tanzania na wala sikuwa na taarifa zake. Kwa hiyo kati ya hawa watatu waliotoweka na ambao hatujui kama wamekufa au la mmoja alikuwa anapenda sana kutumia alama ya Sungura aliyefumba macho kama alama yake. Bila shaka unaelewa sifa za Sungura; akiwa amefumba macho ina maana hajalala, na macho yakiwa yamefumbuliwa ina maana amelala. Sungura anajiamini kwa mbio fupifupi na haoni shida kuwa jirani na adui maana anajiamini kwa chenga. Hizo ndiyo zilikuwa sifa za huyo kijana wangu. Yeye alikuwa hamkwepi adui hata siku moja, alikuwa akiwasaka na kuwafuata hadui katika himaya zao. Kijana huyu alikuwa mjanja kupindukia, kama Sungura. Kwa hii alama na vitendo vilivyokwisha fanyika, nina hakika kabisa kuwa huyu kichaa yuko hapa mjini. Na kama yuko hapa mjini basi kazi ipo kweli kweli. Inabidi ujipange sawa sawa Sogoyo…..”
“Jina lake halisi anaitwa nani? Inspekta Sogoyo aliuliza
“Mtu akishaondoka kwenye timu na tukawa tunajua ni mtu hatari sana, jina lake linabaki kuwa kitu cha siri ambacho kitafia vifuani mwa wanaojua. Tunafanya hivi ili hata ikitokea akafanya madhambi nchi nyingine hatutaki wamuhusishe na sisi. Huwa tunaharibu jina lake katika kumbukumbu zote ambazo limewahi kuwepo. Hivyo jibu naloweza kukupa ni…sijui jina lake halisi”
“Kwa hiyo kati ya vijana wako safi watano hakuna hata mmoja aliyebaki kuwa msafi? Inspekta Sogoyo alihoji huku akishusha pumzi.
“Aliyemuua Kiroboto mwaka jana yeye ndiye pekee aliyebaki upande wa serikali japo si rahisi kumpata maana hajihusishi na serikali moja kwa moja, mmoja atakuwa ndiyo huyu ambaye unatakiwa ukabiliane naye hapa Arusha sasa, wengine wawili sijui wako wapi na sijui majina yao kama nilivyokuambia. Mmoja ndiyo aliuawa mwaka jana” Edson alisema huku akijinyoosha na kisha kumimina kahawa kwenye kikombe.
“Haina shida nadhani tunaweza kabiliana naye tu, tutamshinda tu. Nikimpata nitamfikishia salamu zako kabla sijaweka risasi ya mwisho kwenye kichwa chake. Maana mijitu kama hiyo ukiipata unaua pale pale halafu unaandaa sababu safi za kuhalalisha kitendo chako” Inspekta Sogoyo aliongea kwa sauti ya jazba kidogo.
“Naomba Mungu mumpate, na kama kweli ukimpata mfikishie salamu kama ulivyosema. Ila najua haitakuwa kazi rahisi, kumbuka hapa mnapambana na mtu mwenye uwezo wa kumaliza kikosi cha jeshi la watu Mia moja yeye peke yake. Ninaposema vijana safi namaanisha walikuwa vijana safi, ambao Nyerere mwenyewe alikuwa anaelewa kuwa ana watu kama hao….”
“Sasa mzee Edson naona unanitisha sasa” Sogoyo alifoka.
“Sikutishi, nakuambia hali halisi, kumjua mpinzani wako inasemekana ni nusu ya ushindi. Nakuambia hivi ili ujue namna ya kupambana na huyu mtu. Hata miye najuta kwa nini niliwaacha hai hawa vijana, nadhani kuwaacha hai lilikuwa ni kosa la kifundi ambalo madhara yake nayaona sasa” Mzee Edson aliongea kwa unyonge na sauti ya kusononeka.
“Tutampata tuu, wala usijali. Miye Sogoyo. Nina timu ya vijana safi ambao kwa pamoja tunaweza utifua mjiu huu juu chini hadi mtu wako apatikane. Labda akimbie mji mambo yakishamkalia vibaya, la, nitakuletea kichwa chake hapa utoe salamu za mwisho!!!!
Inspekta Sogoyo alisema huku akiwa anainuka tayari kwa kuondoka.
“Nani wa kukimbia? Edson aliuliza kwa sauti ya chini
“Huyo mtu wako” Sogoyo alisema
“Inspekta, kuwa makini kijana wangu, unaingia kupambana na fundi hasa” Edson alisema, kisha akaongeza.
“Yule ni mtu ambaye kama anakutaka hata wewe anaweza kukufuata kituoni, ukiwa umezungukwa na askari wako”
“Inaonekana wamfagilia sana huyo mtu wako!!! Sogoyo alisema kwa sauti ya mashaka kidogo.
“Sogoyo, usipoteze moyo wa mapambano, wakati mambo yanapokuwa magumu ndipo tunapoweza kuwatambua watu wagumu pia. Nakutakia mafanikio katika kazi yako, ila kuwa makini sana kwa kila ufanyalo kuanzia sasa” Mzee Edson Kinyaro alisema kisha wakapeana mikono kama ishara ya kuagana.
“Je, wahitaji kubaki na hii karatasi? Sogoyo aliuliza
“Hapana, kwenye kazi zetu tulikuwa hatupendi kukaa na ushahidi bila sababu” Mzee Edson alisema huku akiwa anaifinyanga ile karatasi yenye mchoro wa Sungura aliyefumba macho, akaitupia kwenye moto.
Ilikuwa inagota saa moja kasoro dakika sita jioni wakati ambapo Inspekta Sogoyo alipokuwa akiondoka nyumbani kwa Edson Kinyaro, mkuu wa zamani wa idara ya usalama wa Taifa.
Sogoyo alipoondoka, Edson alijibwaga kwenye moja ya sofa zilizokuwa pale sebuleni, huku akionekana mwingi wa mawazo.
“Shiiiit, Max amekuja Tanzania kutafuta nini!!!!!! Edson alijikuta akiwaza kwa sauti. “Mbona hatari sana, kuna jambo kubwa linaendelea hapa Arusha, Max hawezi kuja Arusha hivi hivi. Mshenzi huyu huwa akianza kuua huwa inakuwa nghumu sana kupata namna ya kumzuia, any way dawa yake ni moja tu……!!!!! Edson aliendelea kuwaza kwa sauti huku safari hii akiwa anajizoa zoa toka pale kwenye sofa alipokuwa amejibwaga hapo awali.
“Ama kweli, hata kama mavi ya kale hayanuki lakini bado ni najisi” Alijisemea mzee Edson huku akinyanyua kikombe cha kahawa.
* * *
Inspekta Sogoyo aliendesha gari taratibu wakati akiwa anapita eneo la Nane Nane jirani na kiwanda kilichokufa cha General Tyres. Kwa jinsi alivyokuwa amekaa nyuma ya usukani ungeweza dhani ni mtu mwenye raha zake anaelekea sehemu za burudani kuiridhisha nafsi yake. Akili yake ilikuwa akiwaza mambo mengi wakati simu yake ya mkononi ilipoiita.
“Sogoyo hana naongea”
“Afande kumetokea mauaji tena, safari hii watu watatu wameawa, wanne ni Koplo Maganga” Upande wa pili ulisema.
“Taarifa yoyote ya kutusogeza kwa muuaji? Inspekta Sogoyo alihoji huku akiingiza gia kuliamuru gari liongeze mwendo.
“Hakuna ila ni ajabu sana kwa vile mauji ya safari hii yamefanyika jirani sana na zilipo ofisi zetu afande. Huyu muuaji sijui anajiamini nini, amediriki kufanya mauaji pembezoni mwa majengo ya ofisi za Polisi!!!!!!???? Upande wa pili ulisema kwa sauti ya mshangao iliyochanganyika na mfadhaiko.
“Moto wa makaratasi hauwaki ukakesha, ngoja tuone” Inspekta Sogoyo alisema huku akipangua gia nyingine kwa fujo na kuacha gari ikilalamika na kuongeza mwendo zaidi. Hata alipofika kwenye tuta la pale relini kwenye mchepuko wa kwenda zilipo kotazi za NSSF Njiro wala hakupunguza mwendo. Alipita kiwanda cha Pepsi Njiro akiwa kwende mwendo wa Mia moja na ishirini.
Inspekta Sogoyo aliendesha gari taratibu wakati akiwa anapita eneo la Nane Nane jirani na kiwanda kilichokufa cha General Tyres. Kwa jinsi alivyokuwa amekaa nyuma ya usukani ungeweza dhani ni mtu mwenye raha zake anaelekea sehemu za burudani kuiridhisha nafsi yake. Akili yake ilikuwa akiwaza mambo mengi wakati simu yake ya mkononi ilipoiita.
“Sogoyo hana naongea”
“Afande kumetokea mauaji tena, safari hii watu watatu wameawa, wanne ni Koplo Maganga” Upande wa pili ulisema.
“Taarifa yoyote ya kutusogeza kwa muuaji? Inspekta Sogoyo alihoji huku akiingiza gia kuliamuru gari liongeze mwendo.
“Hakuna ila ni ajabu sana kwa vile mauji ya safari hii yamefanyika jirani sana na zilipo ofisi zetu afande. Huyu muuaji sijui anajiamini nini, amediriki kufanya mauaji pembezoni mwa majengo ya ofisi za Polisi!!!!!!???? Upande wa pili ulisema kwa sauti ya mshangao iliyochanganyika na mfadhaiko.
“Moto wa makaratasi hauwaki ukakesha, ngoja tuone” Inspekta Sogoyo alisema huku akipangua gia nyingine kwa fujo na kuacha gari ikilalamika na kuongeza mwendo zaidi. Hata alipofika kwenye tuta la pale relini kwenye mchepuko wa kwenda zilipo kotazi za NSSF Njiro wala hakupunguza mwendo. Alipita kiwanda cha Pepsi Njiro akiwa kwende mwendo wa Mia moja na ishirini.
* * *
“Unamwona afande wako huyo anapita, nadhani kishapewa taarifa za mapigo mengine. Namuhurumia anaweza vua nguo huyo. Hajui kuwa anacheza na maji yaliyomzidi kimo na ufundi wa kuyaogelea. Ha ha ha ha Nyani hurukia miti yote,lakin sio wa miba” Jamaa huyu alisema kwa majivuni baada ya wao kuiona gari ya Inspekta Sogoyo ikiwa inapita hapo maeneo ya Nane Nane. Walikuwa ndani ya moja ya vyumba vya biashara eneo hilo ambalo linatazamana na kiwanda cha Fibre Board, wote walimwona Inspekta Sogoyo wakati anapita kuelekea nyumbani kwa Edson Kinyaro. Kwa hofu kwamba Inspekta Sogoyo atajua ukweli kuhusu Max, mmoja alipendekeza wammalize kwa kulipua gari ya Inspekta Sogoyo atakapopita wakati akienda kwa Edsoni Kinyaro. Lakini Max alikataa hilo wazo.
“Najua mzee Edson hawezi kumpa askari Polisi taarifa zozote za siri. Sababu ni nyingi lakini pia anajua wazi kuwa Inspekta hawezi kukabiliana na mimi hata akija na jeshi lake zima. Hivyo kumpa jina langu na hata sura yangu anajua fika atakuwa anasaidia kufanya mauaji badala ya kutatua tatizo” Max alisema huku akiendelea kusafisha bastola yake ambayo alikuwa ameisambaza mezani vipande vipande. Baada ya maelezo hayo wenzake wanne aliokuwa nao kwenye chumba hicho walibaki kimya wakimuangalia.
“Haina shida, najua namna tutakavyomchukua Inspekta Sogoyo” Max aliwaondoa wasi wasi wenzie.
“Najua mzee Edson hawezi kumpa askari Polisi taarifa zozote za siri. Sababu ni nyingi lakini pia anajua wazi kuwa Inspekta hawezi kukabiliana na mimi hata akija na jeshi lake zima. Hivyo kumpa jina langu na hata sura yangu anajua fika atakuwa anasaidia kufanya mauaji badala ya kutatua tatizo” Max alisema huku akiendelea kusafisha bastola yake ambayo alikuwa ameisambaza mezani vipande vipande. Baada ya maelezo hayo wenzake wanne aliokuwa nao kwenye chumba hicho walibaki kimya wakimuangalia.
“Haina shida, najua namna tutakavyomchukua Inspekta Sogoyo” Max aliwaondoa wasi wasi wenzie.
Max ama The Fuse kama mzee Edson alivyosema, alikuwa mmoja wa vijana watano waliofuzu mafunzo ya juu kabisa ya ufundi wa kupigana na ujasusi. Utakuwa sawa kapisa kama kwa sasa ungeweza kumwita the world class assassin. Max mwenyewe hujifariji siku zote kwa kusema kuwa; kuna tofauti ndogo sana kati ya malaika na shetani. Mwanzo wote walikuwa malaika, wakati wengine wakibaki malaika hawa wengine wakataka kuwa malaika huru na hivyo jina lao likabadirika kuwa shetani. Kwa vile hawako katika sharia za Mungu. Malaika anaweza kuwa Shetani ila shetani hawezi kuwa malaika wa Mungu tena. Hiyo ndiyo tofauti ya wapelelezi (Spies) na wauaji (Assassin). Hakujutia kitendo chake cha kuasi kwani kwa mtazamo wake kimemfanya kuwa huru na kutumia ufundi wake kwa kiwango cha juu zaidi.
Tangu alipoasi miaka ile, Max alitumia muda mwingi akiwa nchini Zaire na kuwa moja kati ya vifaa vya karibu vya mkono wa kushoto, si wa kulia, wa kushoto wa Raisi wa wakati huo Mobutu Ssseseko. Tangu kufa kwa Mobutu hadi miaka ya karibuni Max alikuwa ameshashuhudia mambo mengi ana mabadiliko mengi sana nchini Congo DRC ambalo ni jina jipya iliyobatizwa nchi hiyo. Kwa muda wote huo ameweza kujifunza kuwa ujasusi ndiyo huongoza nchi, kuchagua maraisi na hata kubadili majina ya nchi. Japo wengi huamini kuwa nchi huongozwa na Raisi na Katiba ambayo hupewa uhai na Bunge, lakini uzoefu wake unamwambia kuwa kila nchi ina kitengo cha ujasusi na hivyo ndiyo huliongoza taifa na kumwambia Raisi nini cha kufanya. Mwaka 1971 alishuhudia jinsi Joseph Désiré Mobutu alivyobadili jina lake kuwa Mobutu Sese Seko hakuishia hapo tu, kwa sababu zile zile za kijasusi zilizomfanya abadili jina lake mwenyewe mwaka huo huo akalazimika kubadili jina la nchi toka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuiita Zaire. Hapo akaridhika na kuiendesha nchi. Lakini pia jenerali Kabila alipoichkua nchi mwaka 1997 kwa sababu zile zile za kijasusi akaamua kurudisha jina la awali na sasa haiitwi tena Zaire bali Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Tangu alipoasi miaka ile, Max alitumia muda mwingi akiwa nchini Zaire na kuwa moja kati ya vifaa vya karibu vya mkono wa kushoto, si wa kulia, wa kushoto wa Raisi wa wakati huo Mobutu Ssseseko. Tangu kufa kwa Mobutu hadi miaka ya karibuni Max alikuwa ameshashuhudia mambo mengi ana mabadiliko mengi sana nchini Congo DRC ambalo ni jina jipya iliyobatizwa nchi hiyo. Kwa muda wote huo ameweza kujifunza kuwa ujasusi ndiyo huongoza nchi, kuchagua maraisi na hata kubadili majina ya nchi. Japo wengi huamini kuwa nchi huongozwa na Raisi na Katiba ambayo hupewa uhai na Bunge, lakini uzoefu wake unamwambia kuwa kila nchi ina kitengo cha ujasusi na hivyo ndiyo huliongoza taifa na kumwambia Raisi nini cha kufanya. Mwaka 1971 alishuhudia jinsi Joseph Désiré Mobutu alivyobadili jina lake kuwa Mobutu Sese Seko hakuishia hapo tu, kwa sababu zile zile za kijasusi zilizomfanya abadili jina lake mwenyewe mwaka huo huo akalazimika kubadili jina la nchi toka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuiita Zaire. Hapo akaridhika na kuiendesha nchi. Lakini pia jenerali Kabila alipoichkua nchi mwaka 1997 kwa sababu zile zile za kijasusi akaamua kurudisha jina la awali na sasa haiitwi tena Zaire bali Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Na sasa Max yuko Tanzania, Arusha, kwa kazi maalum kama mwenyewe anavyosema.
“Najua afande kisha changanyikiwa hadi sasa. Nyie endeleeni na shughuli nyingine na kupata muda wa kupumzika. Kazi tuliyofanya hadi sasa inaridhisha sana. Nitawapa taarifa wakubwa kuwa tumeshaanza kuitingisha Arusha, lakini najua hata kabla sijawapatia watakuwa wameshaanza kuzipata kupitia vyombo vya habari. Kwa sasa macho yangu na masikio yangu mawili nayaelekeza kwa Mzee Edson Kinyaro. Najua atakuwa ameshajua kuwa niko hapa mjini kutokana na alama fulani ambayo nimekuwa nikiiacha katika maeneo ya tukio. Katika wapelelezi wote tunaotakiwa kuwaua, kazi kubwa itakuwa namna ya kumuua Jacob Matata. This is my old friend, work mate na pia mwalimu wetu ni mmoja. Ila najua namzidi uzoefu, yeye ameendelea kuwa malaika wakati miye ni shetani sasa. Najua Edson anajua kama kuna mtu wa kuweza kunidhibiti miye kwa lolote nililokusudia kufanya, japo hajui ni nini nataka kufanya, basi mtu huyo ni Jacob Matata. Hatutakiwi kuwauwa Inspekta Sogoyo na Edson Kinyaro kwa sasa. Inspekta Sogoyo tunamwacha hai ili aendelee kueneza habari zetu. Edson tunamwacha ili atusaidie kupata nyendo za Jacob Matata. Akishatuletea tu Jacob Matata basi tunammaliza Edson na Matata pamoja. Nadhani hadi hapo tutakuwa tumemaliza kazi kwa awamu ya kwanza” Max alielezea, wakati huu alikuwa ameshamaliza kusafisha bastola yake.
ITAENDELEA
“Najua afande kisha changanyikiwa hadi sasa. Nyie endeleeni na shughuli nyingine na kupata muda wa kupumzika. Kazi tuliyofanya hadi sasa inaridhisha sana. Nitawapa taarifa wakubwa kuwa tumeshaanza kuitingisha Arusha, lakini najua hata kabla sijawapatia watakuwa wameshaanza kuzipata kupitia vyombo vya habari. Kwa sasa macho yangu na masikio yangu mawili nayaelekeza kwa Mzee Edson Kinyaro. Najua atakuwa ameshajua kuwa niko hapa mjini kutokana na alama fulani ambayo nimekuwa nikiiacha katika maeneo ya tukio. Katika wapelelezi wote tunaotakiwa kuwaua, kazi kubwa itakuwa namna ya kumuua Jacob Matata. This is my old friend, work mate na pia mwalimu wetu ni mmoja. Ila najua namzidi uzoefu, yeye ameendelea kuwa malaika wakati miye ni shetani sasa. Najua Edson anajua kama kuna mtu wa kuweza kunidhibiti miye kwa lolote nililokusudia kufanya, japo hajui ni nini nataka kufanya, basi mtu huyo ni Jacob Matata. Hatutakiwi kuwauwa Inspekta Sogoyo na Edson Kinyaro kwa sasa. Inspekta Sogoyo tunamwacha hai ili aendelee kueneza habari zetu. Edson tunamwacha ili atusaidie kupata nyendo za Jacob Matata. Akishatuletea tu Jacob Matata basi tunammaliza Edson na Matata pamoja. Nadhani hadi hapo tutakuwa tumemaliza kazi kwa awamu ya kwanza” Max alielezea, wakati huu alikuwa ameshamaliza kusafisha bastola yake.
ITAENDELEA
No comments:
Post a Comment