“Inspekta kuna mauaji mengine tena yametoke, Koplo Sahani ameuwawa katika mtindo ule ule wa tukio la asubuhi na mchana huu….”
“Uko wapi?
“Niko eneo la tukio afande”
“Eneo la tukio halina jina au utambulisho? Inspekta alifoka
“Hapa kwenye daraja la mto Arusha jirani na New Arusha Hotel, kabla hujafika mzunguko wa Naaz”
“Nakuja hapo sasa hivi”Sogoyo alisema huku akiparamia ngazi kushuka chini. Ofisi ya Inspekta Sogoyo iko orofa ya pili katika majengo hayo ya Polisi.
Dakika tano baadaye Inspekta Sogoyo alikuwa ameungana na askari wengine waliokuwa eneo la tukio.
“Wewe umesema Koplo Sahani kauwawa mbona hukusema kuwa kuna mtu mwingine kauwawa? Inspekta alimtupia swali Koplo Maganga bila ya kumwangalia usoni, kwani macho ya Inspekta yalikuwa yametuama kwanye maiti mbili zilizokuwa mbele yake. Maiti moja ilikuwa ya Koplo Sahani na nyingine ya raia mmoja, mwanume ambaye alionekana kuwa umri wa kati ya mtu mzima na kijana.
“Kuna lolote la haja ambalo mmeweza baini hapa? Inspekta Sogoyo alihoji huku macho yake yakiwa bado kwenye zile maiti kama mwanzo .
“Hakuna lolote la maana” Koplo Maganga alijibu
“Lisilo la maana je? Aliuliza safari hii macho yake madogo kama ya mchina yakiwa yanamwangalia Maganga.
“Tumekuta mchoro wa Sungura kwenye kiganja cha Koplo Sogoyo, sasa tumeshindwa kuelewa kuwa alijichora mwenyewe au kachorwa na muuaji!!!
“Uko wapi huo mchoro?
“No no no no don’t ever try that, usiguse hata kidogo” Sogoyo alifoka mara baada ya kumuona Koplo Maganga anataka kushika kiganja cha maiti ya Koplo Sanani.
“Kwa mujibu wa ripoti ya madaktari, muuaji anatumia silaha ya kibaologia kwa hivyo ni hatari sana kugusa gusa chochote kwa sasa bila kuwa na kinga, ndiyo maana uchukuaji na utunzaji wa hizi maiti unafanywa na wao wenyewe Madaktari” Inspekta Sogoyo alifafanua.
“Okay, nimeona” Hatimaye Inspekta Sogoyo alisema baada ya Koplo Maganga kutumia kijiti kufunua kiganja cha mkono wa maiti ya Koplo Sahani.
“Hili ni balaa, ila kwa njia yoyote ile lazima huyu mnyama apatikane. Hatuwezi kuendelea kushuhudia huu upuuzi” Maneno yalimtoka Inspekta Sogoyo.
“Bila shaka na wewe utakuwa umepigiwa na mtu usiyemjua kukupa taarifa za mauaji haya?
“Ndiyo afande. Ila miye nilifanikiwa kumuuliza jina, hakunijibu akakata simu? Koplo Maganga alisema huku akiwa anaifunika maiti ya Koplo Sahani.
“Sasa wewe mbona umeleta shuka moja wakati unajua kuna maiti wawili hapa? Inspekta Sogoyo alimuuliza askari mmoja aliyekuwa ameleta shuka ya kufunikia maiti wakati wakisubiri madaktari wafike kwa ajili ya upimaji na ubebaji wa zile maiti.
“Au unadhani kuna ngazi tofauti ya hadhi ya ubinadamu kati ya askari na raia wa kawaida? Wote ni raia, tena nilitegemea ungemfunika raia wa kawaida ambaye tuna jukumu la kumlinda. Ni aibu kwa askari aliyepewa mafunzo kuuawa pamoja raia wa kawaida” Alisema Inspekta Sogoyo, huku askari kadhaa waliokuwa eneo hilo wakiwa wanaangaliana.
“Kama hamna shuka ya ziada, hiyo shuka itumieni kufunika hiyo maiti ya raia wa kawaida” Sogoyo aliamuru hukua akiwa anatembea kutoka kwenye bonde la mto. Sehemu iliyotokea mauaji hayo iko upande wa nyuma wa duka la matairi na vipuri vya magari liitwalo Michellin. Upande wa pili ukivuka barabara juu ya daraja hilo ndipo ilipo hoteli ya New Arusha.
Inspeka Sogoyo alikuwa ameshafika upande wa juu wa bonde hilo sambamba na ukuta wa Michellin, gafula akaropoka.
“Sungura, sasa nimekumbuka!!!! Kwa nini Koplo Sahani alijichora Sungura” Alikimbia kurudi kule chini bondeni.
“Hebu tuone hiyo picha ya Sungura iliyoko kwenye kiganja cha Koplo Sahani” Alisema alipozifikia zile maiti. Kwa vile maiti ya Koplo Sahani ilikuwa haijafunikwa, kwa kutumia kijiti kama awali walikipanua kiganja cha Koplo Sahani. Macho ya askari kadhaa yakawa yanauangalia ule mchoro. Ulionyesha wazi kuwa Sungura alyechorwa alikuwa amefumba macho.
“Okay, mtakumbuka kuwa kule hospitali, alama za viatu vya mtu anayesadikiwa kuwa ni muuaji zilikuwa na picha ya Sungura, mauji ya pili pia yalionyesha unyayo wa kiatu kilichokuwa na picha ya Sungura. Kuna kitu hapa lazima. Ila isiwe shida maana uzuri wa nyavu siku zote ni matundu yake. Samaki anaweza jiona anapita, atashangaa tu mifupa yake imebana” Alisema Inspekta huku akitembea taratibu kwa mwendo wa mtu aliyevaa nguo ya ndani ambayo ni mbichi.
“Uko wapi?
“Niko eneo la tukio afande”
“Eneo la tukio halina jina au utambulisho? Inspekta alifoka
“Hapa kwenye daraja la mto Arusha jirani na New Arusha Hotel, kabla hujafika mzunguko wa Naaz”
“Nakuja hapo sasa hivi”Sogoyo alisema huku akiparamia ngazi kushuka chini. Ofisi ya Inspekta Sogoyo iko orofa ya pili katika majengo hayo ya Polisi.
Dakika tano baadaye Inspekta Sogoyo alikuwa ameungana na askari wengine waliokuwa eneo la tukio.
“Wewe umesema Koplo Sahani kauwawa mbona hukusema kuwa kuna mtu mwingine kauwawa? Inspekta alimtupia swali Koplo Maganga bila ya kumwangalia usoni, kwani macho ya Inspekta yalikuwa yametuama kwanye maiti mbili zilizokuwa mbele yake. Maiti moja ilikuwa ya Koplo Sahani na nyingine ya raia mmoja, mwanume ambaye alionekana kuwa umri wa kati ya mtu mzima na kijana.
“Kuna lolote la haja ambalo mmeweza baini hapa? Inspekta Sogoyo alihoji huku macho yake yakiwa bado kwenye zile maiti kama mwanzo .
“Hakuna lolote la maana” Koplo Maganga alijibu
“Lisilo la maana je? Aliuliza safari hii macho yake madogo kama ya mchina yakiwa yanamwangalia Maganga.
“Tumekuta mchoro wa Sungura kwenye kiganja cha Koplo Sogoyo, sasa tumeshindwa kuelewa kuwa alijichora mwenyewe au kachorwa na muuaji!!!
“Uko wapi huo mchoro?
“No no no no don’t ever try that, usiguse hata kidogo” Sogoyo alifoka mara baada ya kumuona Koplo Maganga anataka kushika kiganja cha maiti ya Koplo Sanani.
“Kwa mujibu wa ripoti ya madaktari, muuaji anatumia silaha ya kibaologia kwa hivyo ni hatari sana kugusa gusa chochote kwa sasa bila kuwa na kinga, ndiyo maana uchukuaji na utunzaji wa hizi maiti unafanywa na wao wenyewe Madaktari” Inspekta Sogoyo alifafanua.
“Okay, nimeona” Hatimaye Inspekta Sogoyo alisema baada ya Koplo Maganga kutumia kijiti kufunua kiganja cha mkono wa maiti ya Koplo Sahani.
“Hili ni balaa, ila kwa njia yoyote ile lazima huyu mnyama apatikane. Hatuwezi kuendelea kushuhudia huu upuuzi” Maneno yalimtoka Inspekta Sogoyo.
“Bila shaka na wewe utakuwa umepigiwa na mtu usiyemjua kukupa taarifa za mauaji haya?
“Ndiyo afande. Ila miye nilifanikiwa kumuuliza jina, hakunijibu akakata simu? Koplo Maganga alisema huku akiwa anaifunika maiti ya Koplo Sahani.
“Sasa wewe mbona umeleta shuka moja wakati unajua kuna maiti wawili hapa? Inspekta Sogoyo alimuuliza askari mmoja aliyekuwa ameleta shuka ya kufunikia maiti wakati wakisubiri madaktari wafike kwa ajili ya upimaji na ubebaji wa zile maiti.
“Au unadhani kuna ngazi tofauti ya hadhi ya ubinadamu kati ya askari na raia wa kawaida? Wote ni raia, tena nilitegemea ungemfunika raia wa kawaida ambaye tuna jukumu la kumlinda. Ni aibu kwa askari aliyepewa mafunzo kuuawa pamoja raia wa kawaida” Alisema Inspekta Sogoyo, huku askari kadhaa waliokuwa eneo hilo wakiwa wanaangaliana.
“Kama hamna shuka ya ziada, hiyo shuka itumieni kufunika hiyo maiti ya raia wa kawaida” Sogoyo aliamuru hukua akiwa anatembea kutoka kwenye bonde la mto. Sehemu iliyotokea mauaji hayo iko upande wa nyuma wa duka la matairi na vipuri vya magari liitwalo Michellin. Upande wa pili ukivuka barabara juu ya daraja hilo ndipo ilipo hoteli ya New Arusha.
Inspeka Sogoyo alikuwa ameshafika upande wa juu wa bonde hilo sambamba na ukuta wa Michellin, gafula akaropoka.
“Sungura, sasa nimekumbuka!!!! Kwa nini Koplo Sahani alijichora Sungura” Alikimbia kurudi kule chini bondeni.
“Hebu tuone hiyo picha ya Sungura iliyoko kwenye kiganja cha Koplo Sahani” Alisema alipozifikia zile maiti. Kwa vile maiti ya Koplo Sahani ilikuwa haijafunikwa, kwa kutumia kijiti kama awali walikipanua kiganja cha Koplo Sahani. Macho ya askari kadhaa yakawa yanauangalia ule mchoro. Ulionyesha wazi kuwa Sungura alyechorwa alikuwa amefumba macho.
“Okay, mtakumbuka kuwa kule hospitali, alama za viatu vya mtu anayesadikiwa kuwa ni muuaji zilikuwa na picha ya Sungura, mauji ya pili pia yalionyesha unyayo wa kiatu kilichokuwa na picha ya Sungura. Kuna kitu hapa lazima. Ila isiwe shida maana uzuri wa nyavu siku zote ni matundu yake. Samaki anaweza jiona anapita, atashangaa tu mifupa yake imebana” Alisema Inspekta huku akitembea taratibu kwa mwendo wa mtu aliyevaa nguo ya ndani ambayo ni mbichi.
* * *
Dakika ishirini baadaye ilikuwa imefika saa Kumi na moja kasoro dakika sita jioni ya siku hiyo hiyo ya Alhamisi Julai 16, 2009, Inspekta Sogoyo alikuwa na jalada jipya kabisa ambalo lilikuwa limebeba karatasi kadhaa. Vituko na mauaji yaliyokuwa yameanza kutokea asubuhi hiyo walikuwa wameshayafungulia jalada. Jalada hilo kwa sasa lilikuwa na ripoti za madaktari kuhusu matoke ya vipimo ya maiti waliokuwa wamekufa mpaka wakati huo. Pia kulikuwa na taarifa za Polisi kuelezea matukio yalivyotokea na ushahidi mbali mbali uliokuwa umepatikana mpaka muda huo.
Kwa mujibu wa kitengo cha habari na mawasiliano cha jeshi la Polisi mkoa, ilionyesha kuwa mpigaji wa simu aliyewapigia Koplo Sahani na Koplo Maganga alikuwa ni mmoja japo alitumia namba tofauti. Lakini pia iligundulika kuwa mpigaji wa simu, mara zote aliwapigia Polisi akiwa ama jirani sana na eneo la tukio au katika eneo la tukio kabisa.
“Sungura akiwa amefumba macho, maana yake hajalala, yuko macho na makini kabisa kwa lolote” Inspekta alijisemea katika hali ya kutafuta sababu hasa ya Koplo Sahani kujichora picha ya Sungura akiwa amefumba macho! Inspekta Sogoyo alihisi jasho likiyatekenya makwapa yake japo kulikuwa na hali ya baridi kali. Akatoa kitambaa mfukoni na kufuta paji lake la uso ambapo kulikuwa na ile jasho nyembamba ya baridi. Jasho ambayo inamudu kuipenya ngozi ya baridi kutokana na msukumo mkubwa wa damu unaofanyika ndani ya mwili inayoletelezwa na muhusika kutingwa na mawazo mengi!!!!
“Ama kweli ukiamua kuuza utumbo basi usiogope kufuatwa na Inzi” Sogoyo alijisemea huku bado akiwa anatajaribu kutafakari nini maana ya Sungura aliyefumba macho. Aliinua mkonga wa simu ya mezani iliyokuwa upande wa kushoto wa meza yake. Alibonyeza namba kadhaa, ambazo hakuhitaji kuangalia mahali kwani inaonyesha alikuwa nazo kichwani.
“Ndiyo mzee Edson. Habari za siku mzee wangu? Inspekta Sogoyo alisalimia baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
* * *
Dakika ishirini baadaye ilikuwa imefika saa Kumi na moja kasoro dakika sita jioni ya siku hiyo hiyo ya Alhamisi Julai 16, 2009, Inspekta Sogoyo alikuwa na jalada jipya kabisa ambalo lilikuwa limebeba karatasi kadhaa. Vituko na mauaji yaliyokuwa yameanza kutokea asubuhi hiyo walikuwa wameshayafungulia jalada. Jalada hilo kwa sasa lilikuwa na ripoti za madaktari kuhusu matoke ya vipimo ya maiti waliokuwa wamekufa mpaka wakati huo. Pia kulikuwa na taarifa za Polisi kuelezea matukio yalivyotokea na ushahidi mbali mbali uliokuwa umepatikana mpaka muda huo.
Kwa mujibu wa kitengo cha habari na mawasiliano cha jeshi la Polisi mkoa, ilionyesha kuwa mpigaji wa simu aliyewapigia Koplo Sahani na Koplo Maganga alikuwa ni mmoja japo alitumia namba tofauti. Lakini pia iligundulika kuwa mpigaji wa simu, mara zote aliwapigia Polisi akiwa ama jirani sana na eneo la tukio au katika eneo la tukio kabisa.
“Sungura akiwa amefumba macho, maana yake hajalala, yuko macho na makini kabisa kwa lolote” Inspekta alijisemea katika hali ya kutafuta sababu hasa ya Koplo Sahani kujichora picha ya Sungura akiwa amefumba macho! Inspekta Sogoyo alihisi jasho likiyatekenya makwapa yake japo kulikuwa na hali ya baridi kali. Akatoa kitambaa mfukoni na kufuta paji lake la uso ambapo kulikuwa na ile jasho nyembamba ya baridi. Jasho ambayo inamudu kuipenya ngozi ya baridi kutokana na msukumo mkubwa wa damu unaofanyika ndani ya mwili inayoletelezwa na muhusika kutingwa na mawazo mengi!!!!
“Ama kweli ukiamua kuuza utumbo basi usiogope kufuatwa na Inzi” Sogoyo alijisemea huku bado akiwa anatajaribu kutafakari nini maana ya Sungura aliyefumba macho. Aliinua mkonga wa simu ya mezani iliyokuwa upande wa kushoto wa meza yake. Alibonyeza namba kadhaa, ambazo hakuhitaji kuangalia mahali kwani inaonyesha alikuwa nazo kichwani.
“Ndiyo mzee Edson. Habari za siku mzee wangu? Inspekta Sogoyo alisalimia baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
* * *
Kati ya sehemu zilizojengeka vema katika jiji la Arusha basi ni upande wa nyuma ya mlima kilipo chuo utawala cha nchi za Kusini na Mashariki ya Afrika – ESAMI. Ukifika eneo hilo utatamani kushinda hapo ukiangalia nyumba za kifahari ambazo zimeoteshwa kama uyoga. Maeneo hayo ndipo anapoishi mtu ambaye Inspekta Sogoyo alikuwa amempigia simu. Mtu mwenyewe anaitwa Edson Kinyaro. Wakati simu iliyopigwa na Inspekta Sogoyo inaingia, Edson Kinyaro alikuwa amepumzika nyumbani. Umri wa miaka Sitini na Tisa na hali ya hewa ya Arusha siku hiyo ilikuwa ni sababu tosha ya kumfanya ajikunyate kwenye jiko lake la Dohani akiwa anaota moto.
“Vipi kijana, mbona sauti yako inaonyesha kuna jambo limekukalia vibaya? Mzee Edson alihoji baada ya kupokea simu ya Inspekta Sogoyo
“Kwani hujasikia mzee? Inspekta Sogoyo alihoji
“Nimesikia, lakini si ndiyo kazi yako kijana. Yasipokuwepo hayo na uhalali wa wewe kuwekwa juu ya kikosi cha askari kadhaa walio na dhana na vifaa unakuwa batili” Edson alisema, huku macho yake yakiwa yanang’aa. Alishahisi kuwa kuna jambo kubwa la kiufundi linamtatiza Inspekta Sogoyo. Inspekta Sogoyo hakuwa mgeni kwake, aliujua ujasiri na ushupavu wa Sogoyo, binafsi alimwona kama mmoja wa vijana ambao jeshi la Polisi linafaa kujivunia kuwa nao. Lakini kumsikia Inspekta Sogoyo anaongea kwa sauti ya namna hii, ilimtia shaka Edson Kinyaro.
“Inspekta, najua kuna mauaji yametokea asubuhi na bado yanaendelea kutokea. Raia wanauwa, askari wanauwa, lakini hizo ni changamoto za kazi, na kutatua masuala kama hayo ndiyo kunakupa uzoefu na promosheni kazini. Sisemi tuombee majanga yatokee ili watu mpate uzoefu wa kazi na kupandishwa vyeo baada ya kuyatatua, la hasha, ila wakati ule tunawafundisha tulikuwa tunawaandaa kwa mambo kama haya” Mzee Edson alisema huku akiwa anajitengeneza vema pale alipokuwa amekaa.
“Sikiliza mzee wangu, nahitaji kuongea na wewe maana kuna kitu ambacho nahisi unaweza nisaidia ili kutatua. Siyo kuwa naogopa shida, unanijua vema, inapokuja suala la kutetea raia, niko tayari kuifuata mauti ilipo na kupambana nayo. Ila kuna kitendawili ambacho najua kinahitaji siku nyingi kukitegua ila kwa ufundi ulionao na uzoefu wako najua waweza kuwa na walau mwanga juu ya hiki kitendawili….”
“Kitendawili gani tena hicho Sogoyo? Miye nimeshatundika viatu aisee sitaki tena kuingia kwenye hayo mambo, tena mambo yenyewe ya kipolisi. Kumbuka sikuwahi kuwa Polisi, muda wangu wote nimefanya kazi kwenye Usalama wa taifa kama CID” Edson alijitetea
“Nakuja tuongee, sitakuchukulia muda wako mwingi…nadhani waelewa kuna mambo hatuwezi ongea kwenye simu….SUNGURA ALIYEFUMBA MACHO Mzee wangu, ndiyo kitendawili chenyewe. Haya naja sasa hivi” Inspekta alisema kwa kushusha pumzi nyingi kwenye kiwambo cha kupokelea sauti cha ule mkono wa simu.
“Haaaaaaaaah toba, Sungura aliyefumba macho!!!!!!! Hapo kazi ipo haya njoo unisimulie nisikie” Simu ilikatwa.
Dakika tano baadaye, gari ya Inspekta Sogoyo ilikuwa inaegeshwa kwenye uwa wa ndani wa nyumba ya Edson Kinyaro.
“Karibu kijana, keti kitini” Edson Kinyaro alikaribisha baada ya Inspekta Sogoyo kuwa ameingia ndani.
“Asante mze, naona wajibanika tu motoni hapo”
“Nitafanyaje mwanangu, hii hali ya hewa na umri huu basi inakuwa shida kweli kweli!!!
“Ila una mwili mzuri sana Mzee Edson, unajua mtu akiangalia mwili wako hawezi amini kuwa unabeba miaka uliyonayo. Unaoneka mtu wa kati ya miaka arobaini na tano hadi hamsini hivi”
“Aaaaah nashukuru, ila tofauti naiona kwenye uwiano wa akili na vitendo. Akili bado inauwezo wa kuwaza kwa kasi lakini mwili unashindwa kuendana na kasi ya akili, hapo ndipo najua miye siyo yule Kinyaro ambaye watu walikuwa wakihangaika kuonana na miye miaka ile nikiwa kazini”
“Aaah ha ha ha ha” Wote walicheka
“Ndiyo niambie kijana, kuna nini kinakusibu?
“Aaaah mzee wangu si unajua Visima vya kale havifukiwi! Inspekta Sogoyo alisema huku akikunjua karatasi fulani nyeupe.
“Kuna hii picha” Inspekta Sogoyo sasa alisema huku akikabidhi karatasi iliyokuwa na mchoro.
“Leo asubuhi baada ya mauaji ya pale hospitalini, kati ya alama ambazo vijana wangu waliweza kuzipata eneo la tukio ni alama ya soli ya kiatu. Alama hii ilipatika eneo ambalo ulikutwa mwili wa mlinzi wa hospitali. Lakini pia alama hii ya viatu iliishia sehemu ambayo gari lililokuwa limebeba wauaji lilikuwa limeegeshwa. Alama hii pia imekutwa sehemu ambayo tuliukuta mwili wa raia aliyeuwawa mchana wa leo hii hii kule maeneo ya Sakina. Alama hii hii tumeikuta tena sehemu ambayo tumezikuta maiti za Koplo Sahani na raia mwingine waliouawa alasiri hii. Kilichonifanya nitilie maanani alama hii ya Sungura aliyefumba macho ni pale tulipokuta Koplo Sahani ambaye pia ameuawa alikuwa ameichora alama hii kwenye kiganja chake cha mkono” Alipofia hapo, Inspekta Sogoyo alivuta pumzi, huku akiwa anaminya minya vidole vyake. Muda wote huo, Edson Kanyaro alikuwa ameshaiweka pembeni ile karatasi akawa anamsikiliza Inspekta Sogoyo, bila kumuangalia macho yao wote yalikuwa yameelekezwa kwenye moto.
“Nimejaribu kuunganisha hii picha na tukio lolote au taarifa yoyote lakini sijafanikiwa. Kwa taarifa nilizo nazo hakuna kampuni ambayo inatengeneza viatu vyenye soli yenye picha ya Sungura. Hivyo kuna uwezokano mkubwa kuwa picha hii ni maalumu na inatambulisha kitu fulani. Na inawezekana inabeba ujumbe Fulani toka kwa yeyote aliye nyuma ya matukio haya” Inspekta Sogoyo alizidi kueleza kwa tuo kama mtu ajielezaye mbele ya Daktari.
“Nimefikiria mtu anayeweza kunipa mwanga wa hili suala, nikapata majina mawili. Moja ni wewe na jingine ni mkuu wa usalama wa taifa aliyeko sasa baada ya wewe kustaafu. Mkuu aliyeko sasa ni mtu mwenye majivuni makubwa hivyo sijawa huru kumuomba ushauri wake, nimekimbilia kwako” Sogoyo alisema huku akiwa anamwangalia Edson kwa upande wa kulia. Mzee Edson hakujibu kitu, aliinuka toka kitini na kuelekea chumbani. Baada ya kama dakika tano alirejea.
“Mzee naona hujabadilika kabisa, tabia zako bado ni zile zile kama wakati ule ukiwa kitengoni” Sogoyo alisema baada ya mzee Edson kuwa amerejea toka chumbani. Alikuwa kimya tena kwa muda bila kusema neno.
“Sogoyo, mtu anayefanya haya mauaji ni moja kati ya watu waliokuwa vijana wangu wa kutegemewa katika idara ya Usalama wa Taifa miaka ile. Lakini kwa sababu ya tamaa ya pesa aliasi na kukimbilia Zaire ya wakati huo ambayo sasa ni Congo DRC. Kutokana na uwezo wake na ufundi wa kupigana na mambo ya kijasusi, Raisi wa wakati ule, Mobutu Sseseko alimchukua na kumfanya kuwa miongoni mwa watu wake wa siri.” Hatimaye Edson alisema safari hii akiwa anamwangalia Sogoyo machoni.
“Vijana wanne kati ya watano niliokuwa nao, walikuwa wanapenda kutumia alama ya wanyama kama utambulisho wao. Kijana mmoja tu hakuwa anatumia utambulisho kama huo. Nasikitika kusema kuwa vijana wengine wawili walikuja kutoweka baadaye, hadi leo hii haijulikani wako wapi. Hatujui kama wamekufa au wako hai. Mmoja aliyekuwa anatumia alama ya Paka aina ya Amazon yaani Amazon Cat [Soma Kitabu cha riwaya ya Heka Heka utamwona huyu] yeye alipoenda kwenye mafunzo ya juu zaidi hakurudi na wala hatukuwa na taarifa zake hadi alipoibuka mwaka jana katika kile kisa cha kusisimua HEKA HEKA. Nadhani unaelewa namwongelea nani? Mzee Edson alimkazia macho Sogoyo.
“Unamwongelea yule Jasusi aliyeuwawa mwaka jana katika lile tukio la kuiba meno ya Tembo?
“Ndiyo huyo huyo” Edson aliitikia
“Ndiyo, sikuwa namjua kabla ila baada ya kuuwawa na Jacob Matata, ndiyo nikajua kuwa alikuwa naitwa Ben au Kiroboto!!!! Inspekta Sogoyo alisema.
“Basi huyo pia alikuwa kijana wangu japo alipokwenda kwenye mafunzo ya mwisho hakurudi tena Tanzania na wala sikuwa na taarifa zake. Kwa hiyo kati ya hawa watatu waliotoweka na ambao hatujui kama wamekufa au la mmoja alikuwa anapenda sana kutumia alama ya Sungura aliyefumba macho kama alama yake. Bila shaka unaelewa sifa za Sungura; akiwa amefumba macho ina maana hajalala, na macho yakiwa yamefumbuliwa ina maana amelala. Sungura anajiamini kwa mbio fupifupi na haoni shida kuwa jirani na adui maana anajiamini kwa chenga. Hizo ndiyo zilikuwa sifa za huyo kijana wangu. Yeye alikuwa hamkwepi adui hata siku moja, alikuwa akiwasaka na kuwafuata hadui katika himaya zao. Kijana huyu alikuwa mjanja kupindukia, kama Sungura. Kwa hii alama na vitendo vilivyokwisha fanyika, nina hakika kabisa kuwa huyu kichaa yuko hapa mjini. Na kama yuko hapa mjini basi kazi ipo kweli kweli. Inabidi ujipange sawa sawa Sogoyo…..”
“Jina lake halisi anaitwa nani? Inspekta Sogoyo aliuliza
“Vipi kijana, mbona sauti yako inaonyesha kuna jambo limekukalia vibaya? Mzee Edson alihoji baada ya kupokea simu ya Inspekta Sogoyo
“Kwani hujasikia mzee? Inspekta Sogoyo alihoji
“Nimesikia, lakini si ndiyo kazi yako kijana. Yasipokuwepo hayo na uhalali wa wewe kuwekwa juu ya kikosi cha askari kadhaa walio na dhana na vifaa unakuwa batili” Edson alisema, huku macho yake yakiwa yanang’aa. Alishahisi kuwa kuna jambo kubwa la kiufundi linamtatiza Inspekta Sogoyo. Inspekta Sogoyo hakuwa mgeni kwake, aliujua ujasiri na ushupavu wa Sogoyo, binafsi alimwona kama mmoja wa vijana ambao jeshi la Polisi linafaa kujivunia kuwa nao. Lakini kumsikia Inspekta Sogoyo anaongea kwa sauti ya namna hii, ilimtia shaka Edson Kinyaro.
“Inspekta, najua kuna mauaji yametokea asubuhi na bado yanaendelea kutokea. Raia wanauwa, askari wanauwa, lakini hizo ni changamoto za kazi, na kutatua masuala kama hayo ndiyo kunakupa uzoefu na promosheni kazini. Sisemi tuombee majanga yatokee ili watu mpate uzoefu wa kazi na kupandishwa vyeo baada ya kuyatatua, la hasha, ila wakati ule tunawafundisha tulikuwa tunawaandaa kwa mambo kama haya” Mzee Edson alisema huku akiwa anajitengeneza vema pale alipokuwa amekaa.
“Sikiliza mzee wangu, nahitaji kuongea na wewe maana kuna kitu ambacho nahisi unaweza nisaidia ili kutatua. Siyo kuwa naogopa shida, unanijua vema, inapokuja suala la kutetea raia, niko tayari kuifuata mauti ilipo na kupambana nayo. Ila kuna kitendawili ambacho najua kinahitaji siku nyingi kukitegua ila kwa ufundi ulionao na uzoefu wako najua waweza kuwa na walau mwanga juu ya hiki kitendawili….”
“Kitendawili gani tena hicho Sogoyo? Miye nimeshatundika viatu aisee sitaki tena kuingia kwenye hayo mambo, tena mambo yenyewe ya kipolisi. Kumbuka sikuwahi kuwa Polisi, muda wangu wote nimefanya kazi kwenye Usalama wa taifa kama CID” Edson alijitetea
“Nakuja tuongee, sitakuchukulia muda wako mwingi…nadhani waelewa kuna mambo hatuwezi ongea kwenye simu….SUNGURA ALIYEFUMBA MACHO Mzee wangu, ndiyo kitendawili chenyewe. Haya naja sasa hivi” Inspekta alisema kwa kushusha pumzi nyingi kwenye kiwambo cha kupokelea sauti cha ule mkono wa simu.
“Haaaaaaaaah toba, Sungura aliyefumba macho!!!!!!! Hapo kazi ipo haya njoo unisimulie nisikie” Simu ilikatwa.
Dakika tano baadaye, gari ya Inspekta Sogoyo ilikuwa inaegeshwa kwenye uwa wa ndani wa nyumba ya Edson Kinyaro.
“Karibu kijana, keti kitini” Edson Kinyaro alikaribisha baada ya Inspekta Sogoyo kuwa ameingia ndani.
“Asante mze, naona wajibanika tu motoni hapo”
“Nitafanyaje mwanangu, hii hali ya hewa na umri huu basi inakuwa shida kweli kweli!!!
“Ila una mwili mzuri sana Mzee Edson, unajua mtu akiangalia mwili wako hawezi amini kuwa unabeba miaka uliyonayo. Unaoneka mtu wa kati ya miaka arobaini na tano hadi hamsini hivi”
“Aaaaah nashukuru, ila tofauti naiona kwenye uwiano wa akili na vitendo. Akili bado inauwezo wa kuwaza kwa kasi lakini mwili unashindwa kuendana na kasi ya akili, hapo ndipo najua miye siyo yule Kinyaro ambaye watu walikuwa wakihangaika kuonana na miye miaka ile nikiwa kazini”
“Aaah ha ha ha ha” Wote walicheka
“Ndiyo niambie kijana, kuna nini kinakusibu?
“Aaaah mzee wangu si unajua Visima vya kale havifukiwi! Inspekta Sogoyo alisema huku akikunjua karatasi fulani nyeupe.
“Kuna hii picha” Inspekta Sogoyo sasa alisema huku akikabidhi karatasi iliyokuwa na mchoro.
“Leo asubuhi baada ya mauaji ya pale hospitalini, kati ya alama ambazo vijana wangu waliweza kuzipata eneo la tukio ni alama ya soli ya kiatu. Alama hii ilipatika eneo ambalo ulikutwa mwili wa mlinzi wa hospitali. Lakini pia alama hii ya viatu iliishia sehemu ambayo gari lililokuwa limebeba wauaji lilikuwa limeegeshwa. Alama hii pia imekutwa sehemu ambayo tuliukuta mwili wa raia aliyeuwawa mchana wa leo hii hii kule maeneo ya Sakina. Alama hii hii tumeikuta tena sehemu ambayo tumezikuta maiti za Koplo Sahani na raia mwingine waliouawa alasiri hii. Kilichonifanya nitilie maanani alama hii ya Sungura aliyefumba macho ni pale tulipokuta Koplo Sahani ambaye pia ameuawa alikuwa ameichora alama hii kwenye kiganja chake cha mkono” Alipofia hapo, Inspekta Sogoyo alivuta pumzi, huku akiwa anaminya minya vidole vyake. Muda wote huo, Edson Kanyaro alikuwa ameshaiweka pembeni ile karatasi akawa anamsikiliza Inspekta Sogoyo, bila kumuangalia macho yao wote yalikuwa yameelekezwa kwenye moto.
“Nimejaribu kuunganisha hii picha na tukio lolote au taarifa yoyote lakini sijafanikiwa. Kwa taarifa nilizo nazo hakuna kampuni ambayo inatengeneza viatu vyenye soli yenye picha ya Sungura. Hivyo kuna uwezokano mkubwa kuwa picha hii ni maalumu na inatambulisha kitu fulani. Na inawezekana inabeba ujumbe Fulani toka kwa yeyote aliye nyuma ya matukio haya” Inspekta Sogoyo alizidi kueleza kwa tuo kama mtu ajielezaye mbele ya Daktari.
“Nimefikiria mtu anayeweza kunipa mwanga wa hili suala, nikapata majina mawili. Moja ni wewe na jingine ni mkuu wa usalama wa taifa aliyeko sasa baada ya wewe kustaafu. Mkuu aliyeko sasa ni mtu mwenye majivuni makubwa hivyo sijawa huru kumuomba ushauri wake, nimekimbilia kwako” Sogoyo alisema huku akiwa anamwangalia Edson kwa upande wa kulia. Mzee Edson hakujibu kitu, aliinuka toka kitini na kuelekea chumbani. Baada ya kama dakika tano alirejea.
“Mzee naona hujabadilika kabisa, tabia zako bado ni zile zile kama wakati ule ukiwa kitengoni” Sogoyo alisema baada ya mzee Edson kuwa amerejea toka chumbani. Alikuwa kimya tena kwa muda bila kusema neno.
“Sogoyo, mtu anayefanya haya mauaji ni moja kati ya watu waliokuwa vijana wangu wa kutegemewa katika idara ya Usalama wa Taifa miaka ile. Lakini kwa sababu ya tamaa ya pesa aliasi na kukimbilia Zaire ya wakati huo ambayo sasa ni Congo DRC. Kutokana na uwezo wake na ufundi wa kupigana na mambo ya kijasusi, Raisi wa wakati ule, Mobutu Sseseko alimchukua na kumfanya kuwa miongoni mwa watu wake wa siri.” Hatimaye Edson alisema safari hii akiwa anamwangalia Sogoyo machoni.
“Vijana wanne kati ya watano niliokuwa nao, walikuwa wanapenda kutumia alama ya wanyama kama utambulisho wao. Kijana mmoja tu hakuwa anatumia utambulisho kama huo. Nasikitika kusema kuwa vijana wengine wawili walikuja kutoweka baadaye, hadi leo hii haijulikani wako wapi. Hatujui kama wamekufa au wako hai. Mmoja aliyekuwa anatumia alama ya Paka aina ya Amazon yaani Amazon Cat [Soma Kitabu cha riwaya ya Heka Heka utamwona huyu] yeye alipoenda kwenye mafunzo ya juu zaidi hakurudi na wala hatukuwa na taarifa zake hadi alipoibuka mwaka jana katika kile kisa cha kusisimua HEKA HEKA. Nadhani unaelewa namwongelea nani? Mzee Edson alimkazia macho Sogoyo.
“Unamwongelea yule Jasusi aliyeuwawa mwaka jana katika lile tukio la kuiba meno ya Tembo?
“Ndiyo huyo huyo” Edson aliitikia
“Ndiyo, sikuwa namjua kabla ila baada ya kuuwawa na Jacob Matata, ndiyo nikajua kuwa alikuwa naitwa Ben au Kiroboto!!!! Inspekta Sogoyo alisema.
“Basi huyo pia alikuwa kijana wangu japo alipokwenda kwenye mafunzo ya mwisho hakurudi tena Tanzania na wala sikuwa na taarifa zake. Kwa hiyo kati ya hawa watatu waliotoweka na ambao hatujui kama wamekufa au la mmoja alikuwa anapenda sana kutumia alama ya Sungura aliyefumba macho kama alama yake. Bila shaka unaelewa sifa za Sungura; akiwa amefumba macho ina maana hajalala, na macho yakiwa yamefumbuliwa ina maana amelala. Sungura anajiamini kwa mbio fupifupi na haoni shida kuwa jirani na adui maana anajiamini kwa chenga. Hizo ndiyo zilikuwa sifa za huyo kijana wangu. Yeye alikuwa hamkwepi adui hata siku moja, alikuwa akiwasaka na kuwafuata hadui katika himaya zao. Kijana huyu alikuwa mjanja kupindukia, kama Sungura. Kwa hii alama na vitendo vilivyokwisha fanyika, nina hakika kabisa kuwa huyu kichaa yuko hapa mjini. Na kama yuko hapa mjini basi kazi ipo kweli kweli. Inabidi ujipange sawa sawa Sogoyo…..”
“Jina lake halisi anaitwa nani? Inspekta Sogoyo aliuliza
ITAENDELEA
No comments:
Post a Comment